Tafuta

Wahamiaji katika fukwe za  visiwa vya Canari nchini Hispania. Wahamiaji katika fukwe za visiwa vya Canari nchini Hispania.   (ANSA)

Papa anawapongeza maaskofu wa Visiwa vya Canari,Hispania

Katika barua ya Baraza la Maaskofu wa Hispania,Baba Mtakatifu anawashauri Kanisa hili kujenga mitandao ya upendo na taa za matumaini ambazo zinaponesha majeraha ya wale ambao wanaanguka.Ametoa mwaliko wa kutafuta nyuso za wahamiaji katika mtazamo ambao unatamani wakati ujao wa amani na udugu.

Na Angella Rwezaula, - Vatican

Kwa kutambua matatizo ya hali mbazo visiwa vya Canari vinapitia kutokana na mgogoro wa wahamiaji, ninapenda kuelekeza baadhi ya maneno ya kuwatia moyo na ya ukaribu. Ndiyo maneno ya Baba Mtakatifu Francisko yanaanza katika barua aliyowatumia Maaskofu wa Visiwa vya Kanari huko Hispania, ambapo Baba Mtakatifu anaelezea shukrani za kwa juhudi zilizofanywa kujibu dharura. Unyeti na ukarimu wenye sifa za wakazi wa Visiwa vya Canari unajionesha hata kwa namna ambayo wanawakaribisha, wanawalinda, wanawahamasisha na kushirikisha kaka na dada ambao wanafika katika fukwe zao kwa utafutaji wa wakati bora ujao, Baba Mtakatifu anaandika katika barua kwa maaskofu wa Baraza la Maaskofu Hispania, iliyochapishwa katika Tovuti rasimi yao.

Kukaribisha wahamiaji ni changamoto

Baba Mtakatifu anasema, Asante kwa ajili ya kufungua milango na moyo  yenu  kwa wale ambao wameteseka. Mwaliko kwa Maaskofu ni kutokana tamanio  mbele ya  zoezi hilo la kichungaji la  kujenga mitandao ya upendo na kuwa taa ya matumaini ili kukabaliana na changamoto za uhamiaji. Yote hayo ni katika matumaini kwamba yanatia nuru katika njia za ubinadamu mpya tayari wa kuinama, kama Msamaria mwema ili kuponya majeraha kwa yule aliyeanguka. Hatimaye Baba Mtakatifu anawashauri kutafuta katika nyuso za wahamiaji, mtazamo mmoja ambao unatamani wakati ujao wa amani na udugu. Kwa kuhitimisha anabainisha kuwa, Tuombe Mungu kwamba matamanio haya yaweze kutimia.

Ujumbe wa Papa kwa maaskofu wa Hispania
21 November 2023, 14:52