Tafuta

Papa ametuma ujumbe wake kwa ajili ya kuombea amani duniani na Nchi Takatifu Papa ametuma ujumbe wake kwa ajili ya kuombea amani duniani na Nchi Takatifu 

Papa ametuma ujumbe kwa njia ya video kuomba amani kwa Ulimwengu na Nchi Takatifu

Katika Ujumbe wa Papa kwa njia ya video uliochapishwa tarehe 22 Novemba 2023 kuombea Dunia na Nchi Takatifu Amani amebainisha kuwa Tuombe kwa sababu migogoro itatuliwe kwa njia ya mazungumzo na majadiliano na si kwa mlima wa vifo kwa pande zote mbili.Tafadhali tusali kwa ajili ya Amani katika Nchi Takatifu.

Na Angella Rwezaula,- Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko  Jumatano tarehe 22 Novemba 2023, ametuma ujumbe wake kwa njia  Video  kwa ajili ya amani. Katika ujumbe huo Baba Mtakatifu anasema, Sisi sote tinahisi uchungu wa Vita. Mnajua mwisho wa vita vya pili vya dunia vita ambavyo, vilishamiri sehemu mbalimbali duniani. Wakati vita vikiwa mbali, labda hatuhisi nguvu zake. Kuna vile ambavyo viko karibu naso  ambavyo vinatufanya tetende: Ukraine na Nchi Takatifu. Ni vizito ambavyo vinatokea Nchi Takatifu. Ni vizito sana. Watu Wapalestina, Watu wa Israeli  wana haki ya amani, wana haki ya kuishi kwa amani: watu wawili ndugu.

Ujumbe wa Papa kwa njia ya video

Baba Mtakatifu Francisko  akiendelea ameongeza kusema kuwa  Tuombe kwa ajili ya Amani  katika Nchi Takatifu. Tuombe kwa sababu migogoro itatuliwe kwa njia ya mazungumzo na majadiliano na si kwa mlima wa vifo kwa pande zote mbili. Tafadhali tusali kwa ajili ya Amani katika Nchi Takatifu. Ujumbe kwa njia yaVideo wa Papa Francisko unahitimishwa.

Ujumbe wa amani wa Papa Francisko kuombea amani Nchi Takatifu
22 November 2023, 16:49