Tafuta

Papa alitembelea Jumuiya ya Cenacolo(yaani Karamu Kuu)mnamo tarehe 18 Agosti 2021. Papa alitembelea Jumuiya ya Cenacolo(yaani Karamu Kuu)mnamo tarehe 18 Agosti 2021. 

Papa apongeza Jumuiya ya Cenacolo kwa miaka 40 ya kutoa huduma!

Pongezi kwa Jumuiya ya Cenacolo kutimiza miaka 40 ya huduma.Salamu kwa Wamisionari wa Mama Yetu wa Mitume wanaofanya Mkutano mkuu.Shukrani kwa Parokia zinazofanya shughuli za kiangazi na watoto na vijana hata mjini Vatican.Papa amewatakia baraka watoto na vijana wa toleo la Tamasha Giffoni.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Mara baada ya tafakari na sala ya Malaika wa Bwana, Dominika tarehe 16 Julai 2023, Baba Mtakatifu Francisko akiwageukia waamini na mahujaji waliofika kwa wingi katika uwanja wa Mtakatifu Petro, amesema kuwa “Kwa moyo mkunjufu, ninatuma salamu zangu kwa Jumuiya ya Cenacolo, ambayo imekuwa mahali pa kukaribisha na kuhamasisha watu kwa miaka 40; Ninambariki Mama Elvira, Askofu wa Saluzzo na ndugu na marafiki wote. Ni kitu kizuri mnachofanya na ni vizuri kuwepo! Asante!

Waamini na mahijaji katika sala ya Malaika wa Bwana
Waamini na mahijaji katika sala ya Malaika wa Bwana   (Vatican Media)

Akiendelea Papa Francisko aidha amesalimu Wamisionari wa Mama Yetu wa Mitume waliokusanyika jijini Roma kwa ajili ya Mkutano wao mkuu. Kadhalika amesalimu wote, waliofika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, Warumi na mahujaji kutoka nchi mbalimbali.

Wanahija, waamini na watawa katika sala ya Malaika wa Bwana
Wanahija, waamini na watawa katika sala ya Malaika wa Bwana   (Vatican Media)

Papa amependa “kuwasalimu na kuwashukuru Parokia zote zinazofanya shughuli za majira ya joto na watoto na vijana katika kipindi hiki hata mjini  Vatican kuna kikundi kimoja ambacho kinathaminiwa sana," Shukrani kwa makuhani, watawa, wahuishaji na familia! alisisitiza.

Vijana wa  Tamasha la filami Giffoni
Vijana wa Tamasha la filami Giffoni

Katika muktadha huo, Papa aliwatakia kila la kheri na baraka kwa toleo lijalo la Tamasha ya Filamu la Giffoni, ambapo wahusika wakuu ni watoto na vijana. Na kwa kuhitimisha amewatakia wote Dominika njema, lakini kama kawaida yake akiwasihi wasisahau kumuombea na yeye anafanya hiyo hivyo!

Baada ya Angelus 16 Julai 2023

 

16 Julai 2023, 13:40