Tafuta

2023.03.27 Kardinali  Karl-Josef Rauber siku ya kuvarishwa  kofia ya ukardinali na Papa Francisko 2023.03.27 Kardinali Karl-Josef Rauber siku ya kuvarishwa kofia ya ukardinali na Papa Francisko 

Salamu za rambi rambi za Papa kwa kifo cha Kard Karl-Josef Rauber

Papa ametuma salamu za rambi rambi kufuatia kifo cha Kardinali Rauber ambaye anamuelezea kama mchungaji wa kweli wa Kanisa.Ni katika telegramu yake aliyoituma kwa Askofu wa Mainz,ambapo Papa Francisko anamkumbuka "kujitoa kwake kwa ajili ya umoja wa watu wa Mungu na kila ishara yake ilikuwa imejaa upendo wa Kristo."

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko ametuma kwa Askofu Peter Kohlgraf, wa jimbo la Mainz, telegramu ya rambirambi kufiatia na kifo cha Kardinali Karl-Josef Rauber, aliyefariki tarehe 26 Machi. Katika telegramu hiyo Papa anabinisha kuwa: "Maisha yake ya kipadre na kiaskofu yalidhihirishwa hasa na utumishi wake kwa mrithi wa Petro", pia  akimkumbuka Kadinali wa Ujerumani katika jitihada za "kujitolea kwake kwa umoja wa watu wa Mungu katika Curia Romana na katika sehemu mbalimbali za dunia kama wa balozi wa Vatican."

Kardinali Karl-Josef Rauber kulia
Kardinali Karl-Josef Rauber kulia

Mchungaji wa kweli wa Kanisa

Baba Mtakatifu aidha ammfafanua Kardinali Rauber kuwa "Kama mchungaji wa kweli wa Kanisa, katika kila ishara yake alijazwa na upendo wa Kristo ambayo ilimfanya asiiweke kwa ajili yake mwenyewe, bali kuipitisha bila kujibakiza na kwa furaha kwa wanadamu." Kwa njia hiyo maombi  ya Papa Francisko ni kwamba marehemu Rauber sasa anaweza "kusifu milele upendo wa huruma ya  Mkombozi".

Kardinali Rauber alimsalimia hata Papa Mstaafu siku alipovikwa mavazi rasmi ya kua Kardinali
Kardinali Rauber alimsalimia hata Papa Mstaafu siku alipovikwa mavazi rasmi ya kua Kardinali

Kufuatia na kifo cha Kardinali Karl-Josef Rauber, Baraza la  Makardinali linaundwa sasa na makadinali 222, kati yao 123 ni wapiga kura na 99 sio wapiga kura.

29 March 2023, 10:45