Tafuta

27-04-2015 Papa Francisko na Profesa  Riccardo Di Segni Mkuu wa Kiyahudi Roma. 27-04-2015 Papa Francisko na Profesa Riccardo Di Segni Mkuu wa Kiyahudi Roma. 

Miaka 10 ya Upapa,Di Segni:Umedumisha uhusiano mwema hata kwa Wayahudi

Matashi yangu kwake Papa Francisko ni kwamba aendelee kuwa na afya,nguvu nyingi,hasa kuwa na hekima na kuendelea kuongoza jumuiya yake kwa nguvu na hekima ambayo amekuwa nayo hadi sasa.Ni matashi mema kutoka kwa Mkuu wa Jumuiya ya Wayahudi Roma kwa ajili ya kumbu kumbu ya miaka 10 ya Papa Francisko

Na Angella Rwezaula; - Vatican.

Matashi mema kwa ajili ya Baba Mtakatifu anayefikisha miaka 10 tangu kuchaguliwa kwake mnamo tarehe 13 Machi 2013, yanaendelea kutolewa hata kutoka kwa  Riccardo Di Segni, Mkuu wa Jumuiya ya Wayahudi Roma, ambaye ameandika kuwa: “Imefika miaka kumi ya Upapa wa Papa Francisko. Namba  10 ni muhimu, ishara, msingi wa mfumo wa kuhesabu; ni vidole kumi vya mikono, lakini pia kwa msomi wa Biblia “10” inakumbusha Amri Kumi, inakumbusha hata maneno kumi msingi ambayo yaliumba ulimwengu na  kwa mujibu wa maneno ya Musa yalikuwa ni maasi ya watu wa Israeli wakati wa kukaa kwao jangwani. Kwa hiyo “10” inakumbusha, kwa maana ya kibiblia, tabia na hata shauku, wakati mwingine  kudhoofisha misingi hii.

Kwa hiyo mkuu wa kiyahudi Roma anabainisha kwamba: “Matashi yangu kwa Papa Francisko ni kwamba aendelea kuwa na afya, nguvu nyingi na hasa kuwa na hekima na kuendelea kuongoza jumuiya yake kwa nguvu na hekima ambayo amekuwa nayo hadi sasa. Na hata ameweza kudumisha uhusiano maalum kwa  urafiki ambao alitaka kuukuza kwa watu wa kiyahudi.”

12 March 2023, 19:40