Papa Francisko:Usiridhike na kidogo,Yesu anakualika kupenda bila kipimo
Angella Rwezaula; - Vatican.
Katika Injili ya liturujia ya Siku,Yesu alisema“msifikiri nilikuja kutengua sheria au Manabii; sikuja kutengua, lakini kuitimiza (Mt 5,17). Kutimiza ndiyo ufunguo wa neno ili kujua Yesu na ujumbe wake. Je nini maana yake? Ili kuelezea Bwana anaanza kusema kile ambacho sio utimilifu. Maandiko yanasema “ usiue, lakini kwa upande wa Yesu hiyo haitoshi ikiwa unaumiza ndugu kwa maneno; Andiko linasema “ usizini “, lakini hiyo haitoshi ikiwa ni kuishi upendo mchafu wa ndumila kuwili na uongo; Andiko linasema“usiape uongo” lakini hiyo haitoshi iwapo ni kusheherekea kuapa baadaye unatenda kwa unafiki (Mt 5,21-37). Kwa namna hiyo hakuna utimilifu. Ndivyo Baba Mtakatifu Francisko, ameanza tafakari yake, Dominika tarehe 12 Februari, kwa waamini na mahujaji waliofika katika uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican.
Baba Mtakatifu Francisko akiendelea na tafakari hiyo amesema : Ili kutoa mfano wa dhati, Yesu anajikita juu ya ibada ya kutoa. Kwa kutoa sadaka kwa Mungu ilikuwa ni kubadilishana bure zawadi zake: ilikuwa ni ibada muhimu sana, kiasi kwamba ilikuwa imekatazwa kuikatiza kama hapakuwapo na sababu kubwa. Lakini Yesu anathibitisha kuwa lazima kuikatiza ikiwa ndugu ana lolote dhidi yetu, awali ni vema kujipatanisha na Yeye (23-24); ni kwa njia hiyo tu ibada inatimilika. Ujumbe huko wazi: Mungu anatupenda kwanza, bure, kwa kuanzisha hatua ya kwanza kuja kwetu bila kustahili; na hivyo sisi hatuwezi kusheherekea upendo wake bila kufanya kwa namna hiyo ya kupiga hatua ya kwanza ya kujipatanisha na yule aliye tujeruhi.
Kuna utimilifu gani mbele ya macho ya Mungu, labda mtazamaji wa nje, ambaye kiukweli ni bure. Kwa maneno mengine Yesu anatufanya kuelewa kuwa sheria za kidini zinahitajika, na ni nzuri, lakini ziko mwanzoni; kwa ajili ya kutoa utimilifu ni lazima kwenda zaidi ya neno na kuiishi maana yake. Amri ambazo Mungu ametupatia zisifungiwe katika usalama safu, uzingativu rasmi, vinginevyo tunabaki katika udini wa nje na uliojitenga, watumishi wa mungu Bwana, badala ya kuwa watoto wa Mungu Baba. Baba Mtakatifu Francisko aidha amesema, shida hii haikuwapo wakati wa Yesu tu, ipo hata leo hii. Wakati mwingine kwa mfano inasikika wanasema: “ Padre mimi sijaua, sijaiba, sijafanya vibaya kwa mtu yeyote…” Ni kama kusema kuwa “mimi niko sawa.”
Ndiyo maana kuna kuridhika na kiwango cha chini kabisa, wakati Yesu anatualika kufanya mengi iwezekanavyo na kupenda bila kipimo kama alivyofanya. Tukumbuke: Mungu hafikiri kwa kuhesabu; Yeye anatupenda kama mpendwa: sio kidogo, lakini kikubwa! Yeye hasemi “ Ninakupenda mpaka sehemu fulani”. Hapana kwa sababu upendo wa kweli hauishi kamwe hadi sehemu fulani na hahisi kamwe sawa; upendo unakwenda zaidi ya, hawezi kufanya kinyume. Bwana alituonesha kwa kutoa maisha yake juu ya msalaba na kwa kusamehe wauaji wake (Lk 23,34). Na alitukabidhi amri ambayo anazingatia “ kuwa tupendane mmoja na mwingine, kama Yeye alivyo tupenda (Yh 15,12). Huo ni upendo ambao unatimiliza sheria, kwa imani na kwa maisha.
Kwa hiyo tunaweza kujiuliza: ninaishije imani? Je, ni suala la mahesabu, taratibu, au historia ya upendo na Mungu? Je, ninatosheka kutofanya ubaya wowote, kuweka “uso wa mbele” mahali pake, au ninajaribu kukua katika upendo kwa Mungu na kwa wengine? Na mara kwa mara ninajihakikisha juu ya amri kuu ya Yesu ambaye ananiomba ikiwa ninampenda jirani kama Yeye anavyonipenda? Kwa sababu wakati mwingine ni rahisi kuhukumu wengine na kusahau kuwa wenye huruma, kama Mungu alivyo kwetu sisi. Mama Maria aliyehifadhi kabisa Neno la Mungu, atusaidie kwenda kutimiza imani yetu na upendo wetu. Papa Francisko amehitimisha.