Tafuta

Hija ya Papa Francisko DRC:Kitovu cha maisha ya watawa ni Yesu!

Papa Francisko akiwa DRC amekutana na mapadre,mashemasi,watawa wa kike na kume na waseminari na amewaalika kumweka Kristo katikati ya maisha yao na kuwa mashuhuda wa furaha ya Injili.Kanisa linawahitaji.Ni katika Siku Kuu ya Kutolewa Bwana Hekaluni sambamba na siku ya Watawa Duniani.Habari katika video fupi na picha.

Na Angella Rwezaula;- Vatican.

Katika Ziara ya kitume ya Baba Mtakatifu Francisko akiwa Congo DRC katika siku ya tatu tangu afikia tarehe 31 Januari,  ambayo ilijaa matukio mengi ya mikutano na hatimaye alikuwa mkutano wa sala katika siku maalum ya ulimwengu.  Na hii ni kwamba kila tarehe 2 Februari ya kila mwaka ni Sikukuu ya Kutolewa kwa Bwana Hekaluni, sambamba na Siku ya Watawa Duniani kote ambapo kwa mwaka huu, Papa akiwa katika ziara yake ya 40 ya kitume katika bara la Afrika,  katika siku yake ya Pili imekuwa fursa kubwa kukutana na mapadre,mashemasi, watawa wa kike na kiume na waseminari katika Kanisa Kuu la Mama Yetu la Congo huko jijini Kinshasa.

Kanisa Kuu la Mama Yetu huko Congo wakati wa mkutano wa sala
Kanisa Kuu la Mama Yetu huko Congo wakati wa mkutano wa sala

Katika tafakari yake  Baada ya kusomwa kwa Injili ambayo ilijikita juu ya kukutana kati ya Simeoni na Mtoto Yesu, Baba Mtakatifu alisema kuwa “Tunapomweka Yesu katikati ya maisha yetu, mtazamo wetu hubadilika, na licha ya juhudi na matatizo yetu yote, lakini tunahisi kufunikwa na nuru Yake, tukifarijiwa na Roho Wake, tukitiwa moyo na Neno lake na kutegemezwa na upendo Wake".

Papa katika Mkutano wa sala na Watawa, makleri, waseminari na mashemasi
Papa katika Mkutano wa sala na Watawa, makleri, waseminari na mashemasi

Baba Mtakatifu Francisko aliwakumbusha watawa wote kwamba, licha ya changamoto nyingi, hata hivyo kuna furaha kuu katika huduma ya Injili. Kwa hiyo alioneza kusema kwamba wakleri na wa watawa wameitwa kuwa mashuhuda wa upendo wa Mungu, kwa kuwapaka watu wake leo  hii mafuta ya faraja na matumaini.

Mkutano wa sala kati ya Papa na makleri, watawa na waseminari
Mkutano wa sala kati ya Papa na makleri, watawa na waseminari

Baba Mtakatifu Francisko vile vile amesisitiza kuwa mapadre, masista, wamisionari na wengine walioitwa katika huduma ya kidini wanaitwa kuwa watumishi wa watu, kufanya kama ishara za uwepo wa Kristo, upendo wake usio na masharti, upatanisho na msamaha wake na huruma yake kwa ajili ya watu wenye mahitaji  na  maskini. Lakini huduma hiyo  alisema, zitakaa daima katika kukabiliana na changamoto na matatizo, ikiwa ni pamoja na hali ya kiroho, faraja ya kidunia, na ujuu juu.

Papa wakati wa Mkutano wa  sala na makleri na watawa
Papa wakati wa Mkutano wa sala na makleri na watawa

Hata hivyo Papa pia alisema kuwa "Changamoto hizi zinaweza kutatuliwa, kwa njia ya maombi, hadharani na faraghani; kwa kujisahau na kujitolea maisha yote kwa wengine; na kwa kuwa walioelimika, waliofunzwa vyema, na wenye shauku mashuhuda wa Injili. Changamoto hizi lazima zikabiliwe ikiwa tunataka kuwatumikia watu tukiwa mashuhuda  wa upendo wa Mungu.

Mkutano wa sala kati ya Papa na Makleri, watawa, waseminari na mashemasi huko DRC

Baba Mtakatifu Francisko kwa kutambua wazi juu ya matatizo wanayokumbana nayo wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, amewakumbusha makleri na watawa juu ya Msamaria Mwema, kusimama kwa ajili ya kuuguza majeraha ya wanyonge. “Kaka na dada huduma ambayo mmeitiwa ndiyo hii hasa, ya kutoa ukaribu na faraja, kama nuru inayoendelea kuangaza katikati ya giza linalozingira”

Papa akiwa mbele ya Picha ya Bikira Maria anasali mara baada ya mkutano wa sala na makleri na watawa wa DRC
Papa akiwa mbele ya Picha ya Bikira Maria anasali mara baada ya mkutano wa sala na makleri na watawa wa DRC

Hata hivyo Papa kwa kutoa shukrani zake za dhati kwa mapadre, mashemasi, watawa wa kike na kiume na  waseminari, aliwahimiza wasivunjike moyo kwa sababu wanahitajika na akaongeza kusema kuwa katika jina la Kanisa zima, wao ni wa thamani na muhimu.  Kwa maana hiyo aliwaalika ili daima wawe  kama mkondo wa  uwepo wa Bwana wenye kufariji, mashuhuda wenye furaha ya Injili, manabii wa amani katikati ya dhoruba za vurugu, wanafunzi wa upendo, walio tayari kutunza majeraha ya maskini na wanaoteseka.

02 February 2023, 19:30