Tafuta

2022.06.03 Barua na Hati za Utambulisho wa Bwana  Rigobert Itoua, Balozi wa Jamhuri ya  Congo 2022.06.03 Barua na Hati za Utambulisho wa Bwana Rigobert Itoua, Balozi wa Jamhuri ya Congo 

Papa amepokea barua na hati za utambulisho wa Balozi wa Congo

Papa amepokea barua na Hati za Utambulisho wa Bwana Rigobert Itoua,Balozi wa Jamhuri ya Congo.

Vatican News

Baba Mtakatifu Francisko  Ijumaa tarehe 3 Juni 2022 amepokea barua na hati za utambulishi wa Balozi wa Jamhuri ya Congo kuwakilisha nchi yake Vatican,  Bwana Rigobert Itoua . Alizaliwa mnamo tarehe 20 Aprili 1947 huko Brazzaville. Ni baba wa familia na watoto sita.

Papa amepokea hati na barua ya Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Congo
Papa amepokea hati na barua ya Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Congo

Mafunzo  

Bwana Rogobert  mnamo 1969 alipata Diploma ya Shule ya sekondari kutoka Seminari ya Mtakatifu  Jean de Brazzaville.  Alipata  pia Leseni ya Fasihi ya Kisasa kutoka Kituo Kikuu cha Mafunzo ya Juu huko  Brazzaville mnamo 1973 na Shahada ya Uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Mahusiano ya Kimatafa huko Cameroon mnamo 1983.

Papa amepokea hati na barua ya Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Congo
Papa amepokea hati na barua ya Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Congo

Nyadhifa

Ameshika nyadhifa  zifuatazo: Profesa katika Chuo cha  Lumumba (1973 - 1977), Mkuu wa Idara ya Asia, MAE (1978 - 1980); Mwambata wa Kidiplomasia katika ofisi ya Urais wa Jamhuri (1983 - 1990); Mshauri, Ubalozi nchini Cuba (1990 - 1995); Naibu Katibu Mkuu nchini mwao, Mkuu wa Idara ya Huduma za Jumla, MAE (1997 - 1998); Naibu Katibu Mkuu, Mkuu wa Idara ya Ushirikiano wa Nchi Mbili, MAE (1998 - 2005); Mshauri, Ubalozi nchini China (2005 - 2010); Balozi, Mkurugenzi wa Baraza la Mawaziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano na Congo Nje ya Nchi (2018 - 2022).

Papa amepokea hati na barua ya Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Congo
Papa amepokea hati na barua ya Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Congo
03 June 2022, 16:55