Tafuta

Kila tarehe 27 ya kila mwaka ni siku ya kimataifa ya kumbu kumbu ya maangamizi ya wayahudi huko  Auschwitz. Kila tarehe 27 ya kila mwaka ni siku ya kimataifa ya kumbu kumbu ya maangamizi ya wayahudi huko Auschwitz. 

Papa Francisko:msiache uendelezwe ukatili mbaya sana usioelezeka!

Papa ametoa wito kwa familia na walimu waweze kukuza ufahamu wa ukurasa mweusi wa historia katika vizazi vipya.Amesema hayo katika muktadha wa mkesha wa Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ya wayahudi ifanyikayo kila ifikapo tarehe 27 Januari ya kila mwaka.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu mara baada ya tafakari na salamu kwa waamini na mahujaji waliokuwa katika Ukumbi wa Paulo VI, Vatican, amekumbusha juu ya siku ya kumbu kumbu ya 77 kimataifa kwa ajili ya waathirika wa mauaji ya kimbari wa kiyahudi ifanyikayo kila ifikapo tarehe 27 Januari ya kila mwaka. Kufuatia na hilo Papa amesema ni lazima kukumbusha maangamizi ya milioni za wayahudi na watu tofauti wa mataifa na imani za kidini.  Hali hii isirudiwe kamwe ya ukatili usiolelezeka. Ametoa wito kwa wote hasa walimu na familia ili waweze kukuza katika vizazi vipya utambuzi wa tishio baya sana katika ukurasa mweusi wa historia. Hiyo haipaswi kusahaulika ili kuweza kujena wakati ujao  mahali ambapo hadhi ya binadamu haikanyagwi tena, amesisitiza.

Auschwitz-birkenau
Auschwitz-birkenau

Hii ni kumbukumbu ya mauaji ya kimbari yalotekelezwa dhidi ya Wayahudi, yaani ‘Holocaust’, ambayo hufanyika  kila mwaka kwa kufunguliwa kwa kambi ya mauaji ya kimbari ya Auschwitz- Birkenau na kumbukumbu kwa wahanga wa mauaji hayo. Tangu wakati huo imebaki  alama ya mauaji ya kimbari yaliyokatiza maisha ya binadamu. Pia mwaka jana, akikumbuka kwenye sala ya Malaika wa Bwana  kuhusu mkasa huo Papa alisema: “Kutojali haukubaliki na kumbukumbu ni wajibu” na  aliwaalika waamini kusali kila mtu moyoni mwake ili janga hili lisitkee tena.

Auschwitz-birkenau
Auschwitz-birkenau

Kwa hakika  kamwe isitokee ingawa ilinyamazishwa kwa kupendelea ukimya wa ufasaha zaidi kuliko kila sentensi au hotuba, na  ishara mbali mbali  zilizotolewa na Papa hasa wakati wa hija yake ya maumivu kwenye kambi  la Auschwitz-Birkenau, mnamo  2016 kwenda Poland. Katika sala mbele ya ukuta wa kunyongwa na mahali ambapo Mtakatifu Maximilian  Maria  Kolbe alikaa dakika za mwisho wa maisha yake, kati ya kukumbatiwa na walionusurika na kutembea akiwa ameinamisha kichwa chake. Papa hakusema neno kutoka kinywani mwake bali ni sala moja tu ilikuwa katika nafsi ya Papa, ile ile aliyoiacha ameandika kwa Kihispania kwenye Kitabu cha Heshima cha kambi ya maangamizi:

“Señor ten piedad de tu pueblo. Señor, perdón por tanta crueldad!, "Yaani Vwaba uhurumie watu wako. Bwana hurumia kwa ukatili mwingi!"

KATEKESI PAPA 26 JANUARI 2022
26 Januari 2022, 13:01