Tafuta

2021.10.22 Akihojiana na Mwandishi Hernán Reyes Alcaide wa Tèlam. 2021.10.22 Akihojiana na Mwandishi Hernán Reyes Alcaide wa Tèlam.  

Papa:Mkutano wa G20 Roma utambue msimamo wa dunia

Katika mahojiano na Shirika la habari la Télam nchini Argentina wamegusia mada ya changamoto nyingi na jinsi ya kuondokana na janga la sasa lakini pia hata uwezekano wa kupanga ziara zake za kitume kama vile kwenda Congo,Hungheria,Papua Guinea Mpya na Timor Est,ziara ambazo bado hazijaandaliwa.

Na Sr. Angella Rwezaula – Vatican.

Katika Mkutano Mkuu wa G20  yaani unaokaribi wa matataifa makuu tajiri ulimwenguni  utakaofanyika Roma, lazima kuwe makini kuchukua maamuzi kwa kuzingatia uhusiano kati ya Nchi ambazo hazijaendelea nazilizo endelea na kutambua msimamo wa ulimwengu kwa mtazamo upatikanaji wa matibabu ya kiafya , ili kushinda vema janga. Huo ni uthibitisho wa Papa Francisko katika mahojiano na a Télam, shirika la Habari la Nchi ya Argentina. Kwa viongozi wa Nchi na Serikali za nchi zilizo tajiri zaidi kwenye sayari  (G20)  Papa anatarajia kwamba mkutano unaweza kusaidia kushusha mivutano kwa ngazi ya ulimwengu mbele ya vurugu zinazoendelea na zinazoibua vurugu zaidi ya vurugu.

Ni kipinidi cha kuondoka nadharia na kutenda

Papa amesema kuwa "Hiki ni kipindi cha kuondoka nadharia na kujikita katika matendo". Akisisitiza zaidi amesema "Mchezo unaochezwa sasa hivi inawezekana kuondokana na janga kwa pamoja. Lazima kuyapa matatizo majina yake yote mawili ambayo yanaukabili ubinadamu katika kipindi baada ya janga. Ni msingi vile vile ambao ni sawa sawa na changamoto zitakazo kabiliwa na COP26 kuhusu tabianchi  huko Glasgow ambao utafanyika mnamo tarehe 12 Novemba".

Ziara za kitume za Papa zijazo

Papa Francisko pia ameelezea kuhusu ziara zake za kitume ambazo anatarajia wakati ujao, kuanzia na ile ya mwezi Desemba huko Ugiriki na Ciprus ambayo tayari imetajwa. Kwa kwa sasa lakini amebainisha ni ziara mbili ambazo hazijapangwa lakini zilizo kwenye akili yake, huko Congo na  Hungheria”, wakati huo huo pia anataka kuzingatia ziara huko Papua Guinea Mpya na Timor Est  zilizohairishwa kipindi cha janga. “Nilifikiri daima ulimwengu wa pembezoni unaonekana wazi  katika miaka saba ya mwisho kamaPapa nimejionea kwa macho yangu mwenyewe”.

Shukrani kwa  Leo Messi

Kwa kufunga baadaye Papa amemshukuru nyota ya mpira wa miguu ya Argentina Lionel Messi, mchezaji sasa wa Paris Saint-Germain, ambaye amehamia Ufaransa, kwa jezi aliyookea katika fursa ta ziara yake Waziri Mkuu  wa Ufaransa Jean Castex, anamshukuru kwa urahisi wake na kwa kumjali. “ Asante kwa ukaribu, kwa ushuhuda kwa kutokugonfisha kichwa  na Mungu akubariki na kuwa na imani daima juu yangu” .

23 October 2021, 16:29