2021.09.09 Papa na Rais wa Jamhuri ya Nchi ya Chile 2021.09.09 Papa na Rais wa Jamhuri ya Nchi ya Chile 

Papa amekutana na Rais wa Chile:Mazungumzo kwa ajili ya wema wa nchi

Umefanyika mkutano wa Papa Francisko na Rais wa Jamhuri ya Chile Bwana Sebastián Piñera Echenique,jijini Vatican na baadaye Kardinali Parolin,Katibu wa Vatican.Mada zilizokabiliwa katika mazungumzo yao ni hali ya nchi,uhusiano na Kanisa,changamoto za sasa kimataifa.Waonesha jitihada kwa ajili ya amani,haki kijamii na ulinzi wa maskini.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Alhamisi tarehe 9 Septemba 2021, Papa Francisko amekutana na Rais wa Jamhuri ya Chile, Bwana Sebastián Piñera Echenique, jijini Vatican, ambaye mara baada ya mkutano huo amekutana pia na Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican, akiambatana na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa  Vatican kwa ajili ya Mahusiano na ushirikiano na Nchi.

Zawadi ya Rais wa Chile kwa Papa
Zawadi ya Rais wa Chile kwa Papa

Katika mazungumzo yao, yameonesha kuwa na uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi hizi mbili, pamoja na jitihada za pamoja kwa ajili ya amani, haki kijamii, ulinzi wa maskini, wahamiaji na watu walio katika mazingira magumu. Wakiendelea na mazungumzo hayo, wametazama hali halisi ya masuala ya ndani ya Nchi huku wakitoa umakini kwa namna ya pakee ya maendeleo, kijamii na kiuchumi, mchakato wa mageuzi ya Katiba na uhusiano na Kanisa katoliki.

Kardinali Parolin na Rais wa Chile
Kardinali Parolin na Rais wa Chile

Kwa mtazamo huo wa sjitahada za Kanisa, ni matarajio ya vionozi hao kuwepo ushirikiano wa utulivu kwa kuzingatia mchango unaotolewa na Kanisa katoliki kwa ajili ya wema wa watu katika muktadha wa upendo, elimu na maisha ya kijamii hasa katika kipindi hiki kigumu cha janga. Mazungumzo yao pia yameruhusu kubadilisha mawazo na mitazamo ya baadhi ya mada zilizopo za sasa kimataifa na kikanda, uhamasishaji wa amani na haki za kibinadamu ulimwenguni.

Zawadi ya Papa kwa Rais wa Chile
Zawadi ya Papa kwa Rais wa Chile

 

09 September 2021, 16:31