2020.11.18 Katekesi ya Papa 2020.11.18 Katekesi ya Papa 

Papa anatoa mwaliko wa kila mmoja kuwa hekalu la Mungu

Papa:Waamini watambue kuishi kwa kujitoa sadaka na sala zao pamoja na mateso yao kama mchango muhimu wa ujenzi wa Kanisa la Bwana,nyumba ya aliyejuu katikati yetu.Amesema hayo Papa mara baada ya katekesi yake Jumatano tarehe 18 Novemba 2020.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican.

Papa Francisko mara baada ya katekesi yake akisalimia waamini wa lugha ya kitaliano amekumbusha kuwa tarehe 18 Novemba siku kuu ya kutabarukiwa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican, na lile la Mtakatifu Paulo nje ya Roma. Siku kuu hiyo iwe na  mwanga muhimu wa Kanisa na jengo takatifu  mahali ambamo wanakusanyika waamini na kuweza kutufanya sisi sote kuwa na utambuzi ya kwamba kila mmoja ameitwa kuwa hekalu la Mungu. Wazo la Papa limewaendea kama wakaida wazee, vijana, wagonjwa na wanandoa wapya. Amewashauri kupenda Kanisa la Bwana; kushirikiana kwa ukarimu na shauku ya ujenzi wake; kuishi kwa kujitoa  sadaka na sala zao pamoja na mateso yao kama mchango muhimu wa ujenzi wa Kanisa la Bwana, nyumba ya aliyejuu katikati yetu” amesisitiza.

 

 

18 November 2020, 16:38