Tafuta

2020.11.25 Katekesi ya Papa Francisko 2020.11.25 Katekesi ya Papa Francisko  

Papa Francisko:katika kipindi hiki kigumu cha Majilio kiwe tumaini kubwa

Katika sala kwa waamini kwa lugha tofauti,mara baada ya tafakari ya Katekesi,Papa Francisko amewaalika kujikita katika kipindi cha sala ya dhati hasa yenye hisia ya kujiadaaa na siku kuu ya kuzaliwa kwa Bwana.

Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican.

Matumaini katika ukweli ambayo yanaokoa, katika mwanga wa nguvu zaidi kwenye giza, ni safari ambayo inabadili moyo. Yote hayo ndiyo majilio. Amesema hayo Papa Francisko mara baada ya Katekesi yake leo hii, tarehe 25 Novemba 2020  akiwakumbusha Kanisa lote  ulimwenguni umuhimu wa maandalizi ya liturujia inayokaribia ya Majilio.  Katika kipindi kigumu kwa walio wengi, tujitahidi kugundua matumaini makuu na furaha ambayo  tulipewa kwa njia ya kuja Mwana wa Mungu ulimwenguni. Amesema hayo  Papa akiwageukia waamini kwa lugha ya kifaransa huku akisisitiza pia juu ya sikukuu iliyopotia ya Kristo Mfalme n wa ulimwengu na kwamba alituokoa dhidi ya  nguvu ya giza na kutuingiza katika ufalme wake ili kuwa mashuhuda waaminifu na ukweli unaookoa.

Papa Francisko akiwasalimia waamini kwa lugha ya Kiitaliano, vile vile amesema Siku kuu ya Kristo Mfalme ambayo tumesheherekea Jumapili, ilihitimisha mwaka wa kiliturujia, na iwezeshe kuwa na utambuzi kwamba Kristo alitukomboa kutoka katika  nguvu za giza, ili kutuingiza katika ufalme wa Mung, na kutufanya sisi kuwa shuhuda amini katika ukweli wa ukombozi. Mawazo yake yamewaendea kama kawaida wazee, vijana, wagonjwa na wanandoa wapya. Kristo ambaye anatawal kutoka Msalabani, awape nguvu wote wakati wa majaribu na mateso kwa kufungua ndani mwao mioyo ya matumaini. Papa Francisko amesalimiwa waamini wanaozungumza lugha ya kiingereza: " wakati tunajiandaa kuingia katika safari ya kipindi cha Majilio mwanga wa Kristo uweze kuonesha njia zetu na kuondoa giza la mioyo yetu". Kwa familia zote amewatakia furaha na amani ya Kristo Yesu.

‎‎‎‏

25 November 2020, 16:05