Covid-19-Jitihada zaidi ulimwenguni zinahitajika hasa kukabiliana na walio wa mwisho, wenye kuhitaji zaidi. Covid-19-Jitihada zaidi ulimwenguni zinahitajika hasa kukabiliana na walio wa mwisho, wenye kuhitaji zaidi. 

Papa Francisko:Suluhisho la usawa katika kipindi cha covid ni muhimu!

Katika sehemu nyingi za ulimwengu,idadi watoto hawawezi kurudi shule,hali hii ina hatari ya kuongezeka kwa ajira kwa watoto,unyonyaji, unyanyasaji na utapiamlo.Kwa kifupi, kutoweza kuona uso wa mtu na kuwachukulia wengine kama wabeba virusi.Ni mfano mbaya wa mzozo wa kijamii ambao lazima uwe wasiwasi kwa wote.Amesema Papa kwa washiriki wa Mkutano wa Taasisi ya Kipapa ya elimu ya sayansi ulioanza tarehe 7 kwa njia ya mtandao.

Na Sr. Angela Rwezaula Vatican

Papa Francisko ametuma ujumbe wake kwa Taasisi ya Kipapa ya elimu ya Sayansi katika Mkutano wao  mkuu uliofunguliwa tarehe 7  na utakaofungwa tarehe 9 Oktoba 2020, mkutano unafanyika kwa njia ya mtandao kutokana na janga la corona au covid-19. Katika ujumbe huo anawasalimia wajumbe wote ambao wanajikita katika  kuweka utafiti  msingi wa kisayansi katika huduma ya afya ya sayari yetu na wakazi wake, hasa maskini na wasiojiweza. Aidha anawasalim wataalam walioalikwa na viongozi, ambao wote wana majukumu mazito ya kimataifa na ambao anatarajia mchango wao. Awali ya yote ameeleza kuunga mkono kwa kazi ya kitaaluma ambayo inahamaishwa na Mwenyekiti Professa Joachim von Braun, na baraza zima. Anatambua kuwa katika shughuli ya mkutano huo kwa siku hizi utakuwa ni kwa ajili ya kutazama yote yanayohusu ubinadamu.

Papa Francisko amesema waanajikita katika masuala ya sayansi katika huduma ya watu kwa ajili ya kuishi binadamu dhidi ya janga la covid-19 na mambo yote yanahusu ulimwengu. Kiukweli, janga hilo limeleta sio tu usalama wetu wa uwongo, lakini pia kutoweza kwa nchi za ulimwengu ili kuweza kufanya kazi pamoja. “Kwa muungano wetu wote tumeshuhudia mgawanyiko ambao ulifanya ugumu wa kupata kusuluhisha shida ambazo zinatuathiri sisi sote (taz. Fratelli Tutti, 7).  Ina maana kubwa kwamba katika mkutano wa mwaka huu kwa njia ya mtandao na ambao unaleta pamoja wajumbe kutoka vitengo mbalimbali vya kisayansi una maana ya kutoa mfano wa jinsi changamoto za mgogoro wa COVID-19 zinavyopaswa kushughulikiwa kupitia juhudi zilizoratibiwa katika huduma ya familia nzima ya wanadamu.

Katika sehemu nyingi za ulimwengu, idadi kubwa ya watoto hawawezi kurudi shule, na hali hii ina hatari ya kuongezeka kwa ajira kwa watoto, unyonyaji, unyanyasaji na utapiamlo. Kwa kifupi, kutoweza kuona uso wa mtu na kuwachukulia watu wengine kama wabeba wa virusi ni mfano mbaya wa mzozo wa kijamii ambao lazima uwe wa wasiwasi kwa wote ambao wana mustakabali wa ubinadamu moyoni., Papa Francisko amesisitiza Katika suala hili, hakuna hata mmoja wetu anayeweza kushindwa kuwa na wasiwasi juu ya athari za mgogoro kwa maskini wa ulimwengu. Kwa wengi wao, suala la  kweli ni moja la kuweza kuishi. Pamoja na mchango wa sayansi, mahitaji ya watu maskini wa familia yetu ya wanadamu wanalalamikia juu ya suluhisho la usawa kwa upande wa serikali na wanatoa maamuzi kwa wote. Mifumo ya utunzaji wa afya, kwa mfano, inahitaji kujumuishwa zaidi na kupatikana kwa wasiojiweza na wale wanaoishi katika nchi zenye kipato cha chini.

Ikiwa mtu yeyote anapaswa kupewa upendeleo, basi iwe nai kwa muhitaji na aliye katika hatari zaidi kati yetu. Vivyo hivyo, chanjo itakapo patikana, ufikiaji e sawa kwao lazima uhakikishwe bila kujali mapato, kila wakati ukianza na uchache. Shida za ulimwengu tunazokabiliwa nazo zinahitaji majibu ya ushirika na pande nyingi. Mashirika ya kimataifa kama UN, WHO, FAO na mengine, ambayo yalianzishwa ili kukuza ushirikiano na uratibu wa ulimwengu, yanapaswa kuheshimiwa na kuungwa mkono ili waweze kufikia malengo yao kwa sababu ya faida ya wote.

Papa Francisko kadhalika amebainisha kuwa mlipuko wa janga hilo, katika muktadha mpana wa ongezeko la joto ulimwenguni, shida ya kiekolojia na upotezaji mkubwa wa bioanuwai, inawakilisha wito kwa familia yetu ya kibinadamu katika kufikiria tena njia yake, kutubu na kufanya uongofu wa kiikolojia (taz. Laudato si - 216-221). Unahitajika uongofu wa kweli ambao kwa kutumia talanta zetu zote tulizopewa na Mungu ili kukuza ikolojia ya wanadamu inayostahili hadhi yetu, na  ya kuzaliwa na hatima . Hili ndilo tumaini nililoelezea katika Waraka wa  wa  hivi karibuni ‘Fratelli Tutti yaani ‘ wote ni ndugu’ juu ya undugu na urafiki wa kijamii. Ingekuwa vizuri Papa amesema kama ukuaji wa uvumbuzi wa kisayansi na teknolojia ungeweza kuja na usawa zaidi na ujumuishaji wa kijamii. Ingekuwa vizuri sana, hata tunapogundua sayari za mbali, kuweza kugundua tena mahitaji ya ndugu kaka  na dada wanaotuzunguka! ” (rej. 31).

07 October 2020, 15:25