2020.10.19 Papa Francisko akutana na Dk Papa Francesco Peter Maurer, Mwenyekiti wa Tume ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu na mwenza. 2020.10.19 Papa Francisko akutana na Dk Papa Francesco Peter Maurer, Mwenyekiti wa Tume ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu na mwenza. 

Mkutano wa Papa na Mwenyekiti wa Msalaba mwekundu kimataifa!

Jumatatu tarehe 19 Oktoba Papa amekutana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu,Dk,Peter Maurer,ambaye akizungumza na vyombo vya habari amesisitiza kuhusu shughuli za Msalaba mwekundu na Vatican hasa msaada kwa ajili ya wathirika wa vita na kutumia nguvu.Amekutana baadaye na Katibu wa Vatican,Kard Parolin.

Migawanyiko yenye kule uchungu  sana  na ambayo inasababaisha athari kwa watu wengi na zaidi walio katika mazingira magumu, kwa ajili ya wahamiaji, uhamisho wa ndani kwa sababu ya vita na kutumia nguvu, kwa ajili ya watu ambao wameambukizwa na harakati ya kununua silaha, mabadiliko ya tabianchi, ukosefu wa maendeleo, ubaguzi umasikini na ukosefu wa haki. Haya yote na masuala mengine mengi zaidi  yameyozungumzwa. Dk.Maurer pia amebainisha juu ya mtazamo wa pamoja wa Papa wenye utashi wa kujenga madaraja kwa ajili ya kukamilisha jamii shirikishi. Hatimaye Dk. Maurer amesisitiza pia kuhusu mada ya Wosia wa “Fratelli tutti” yaani Wote ni ndugu  kwamba inaweza kufikiriwa kama kaulimbiu ya shughuli za Msalaba Mwekundu Kimataifa.

Mahojiano kamili na Mwenyikiti huyo Dk. Peter Maurer yatatakangazwa kesho kupitia  Tovuti ya  Vatican News na Ukurasa wa Gazeti la Osservatore Romano.

19 October 2020, 17:15