Papa kwa walimu katoliki nchini Ufilippino:elimu ishuhudie imani na maadili!
Na Sr. Angela Rwezaula-Vatican
Kuwafundisha vijana na si tu kuwa wanafunzi bora tu, bali pia mashuhuda halisi wa imani. Ndiyo muhtasari wa mwaliko wa Papa Francisko kwa waalimu katoliki wa Ufilipino waliounganika kuanzia tangu 21 na watamaliza 25 Septemba, kwenye Warsha yao ya kila mwaka. Tukio hilo limenadaliwa na Chama cha Elimu Katoliki cha Ufilipino (Ceap), kiungo ambao kinakusanya zaidi ya shule za Kikatoliki 1,500 nchini humo. Kwa sababu ya janga la corona, warsha mwaka huu inafanyika moja kwa moja kupitia tovuti na kwenye mitandao ya kijamii kama vile facebook. Ushauri wa Papa umewafikia kupitia ujumbe uliosainiwa na Katibu wa Vatican Kardinali Pietro Parolin. Ndani mwa ujumbe huo , Papa anakumbusha kwamba elimu Katoliki lazima ifundishe sio tu kufikiria kwa uchambuzi, lakini pia malezi katika mafundisho ya Kikristo na maadili.
Kwa kufanya hivyo itapelekea kuundwa kwa wanaume na wanawake ambao watakuwa tayari kuchukua majukumu makubwa ndani ya jamii na kushuhudia imani ya kweli kwa ulimwengu. Ujumbe wa kipapa ulisomwa na Padri Elmer Dizon, rais wa CEAP, kabla ya kuchaguliwa mwingine ambaye katika hotuba yake ya uzinduzi, hata hivyo alisisitiza jinsi janga hilo lilivyokuwa na athari kubwa kwenye sekta ya elimu. Katika ujumbe wa Papa amesema katikati ya changamoto za sasa juhudi zinazoendelea zinafanywa ilibkuhakikisha kuwa shule Katoliki zinakuwa vichocheo vya mabadiliko.
Kwa upande wake, Monsinyo Roberto Calara Mallari, mjumbe wa Tume ya Maaskofu ya Katekesi na Elimu Katoliki, amehimiza kila shule kuwa ya ubunifu, ili kila mmoja apate njia za kusoma ambazo zinakidhi mahitaji ya wanafunzi wake. Akiendelea amesema na Chama cha Elimu Katoliki cha Ufilipino (Ceap) hakitazuiliwa na woga, lakini kitajitahidi kutenda kama mwongozo kwa wanafunzi na shule ambazo zinajitahidi katikati ya janga hilo. Hatimaye amkumbusha kwamba mada ya Kardinali Luis Antonio Tagle, Rais wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu, inatarajiwa kutolewa siku ya Ijumaa tarehe 25 Septemba 2020. Kama unataka kujiunga unaweza kutmia link hii hapa: https://www.facebook.com/CatholicEdPH/videos/977848552684485