Brazil:Hospitali imekabidhiwa mashine za kupumulia kutoka kwa Papa
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Kwa niaba ya Papa Francsiko, tarehe 17 Agosti 2020 zimetumwa nchini Brazil mashine 18 aina ya Graeger za kupumlia kwenye vyumba vya mahututi pamoja na mashine 6 za ultrasound (aina ya fuji), na ni zawadi ambayo sasa imefika. Vifaa vya kupumulia mapafu na mashine ya uchunguzi katika maabara vimefikishwa katika hospitali ya Mtakatifu Lucas huko Porto Alegre, katika mkoa wa Rio Grande do Sul. Ni moja ya zawadi nyingi kama hizo ambazo Papa Francisko amekwisha toa katika miezi ya hivi karibuni kwa nchi zilizoathiriwa na janga la covid-19 na nchini Brazil ni kati ya zile ambazo kwa muda mrefu zimepata athari nzito ya virusi kwa idadi kubwa ya watu.
Umakini kwa wasio na fursa
Utume wa kutoa msaada wa kibinadamu umeonekana wazi katika jitihada za Mfuko wa Kitume Vatican pamoja na ule wa chama cha Tumaini kisicho cha kiserikali nchini. Katika miji tofauti ya Brazil wanaendelea kupokea vifaa na zana mbali mbali na wakati huo huo Askofu Mkuu Jaime Spengler wa mji wa Porto Alegre, amebariki vifaa vilivyo kabidhiwa katika hospitali ya kizalendona kusisitiza kwamba ishara hiyo ni kielelezo cha mshikamano wa wanaume na wanawake wanaotaabika kutokana na maisha yasiyo na fursa.
Msaada wa kulinda maisha
Mashine za kupumulia na ultrasound vitawekwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi, ambacho kinapokea wagonjwa walio na Covid-19 tu. Kwa mujibu wa Mkuu wa Chuo Kikuu Katoliki cha Kipapa cha Rio Grande do Sul (PUCRS), Padre Evilázio Teixeira, aliyekuwapo wakati wa uwasilishaji wa vifaa hivyo amesema ni ishara ya mshikamano kwa upande wa Kanisa ni muhimu kutoa nguvu kwa utume wao wa utunzaji na kuhamasisha maisha.
Mkoa Rio Grande do Sul
Utafiti kutoka Chuo Kikuu cha Shirikisho la Rio Grande do Sul (UFRGS), kilichochapishwa Jumanne iliyopita, unaonyesha kwamba pigo la maambukizi ya Covid-19 hata hivyo katika mji wa Porto Alegre umepungua, lakini mwenendo wa kesi lazima uendelee kudhibitiwa. Hadi leo hii katika mkoa huo ni watu 115,000 walioambukizwa na vifo zaidi ya elfu tatu wa virusi vya corona!