Papa Francisko:Ukaribu wa Papa kwa watu wanaoteseka na janga!
Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican
Mara baada ya tafakari na sala ya Malaika wa Bwana, Jumapili tarehe 7 Juni 2020, Papa Francisko amewageukia wanahija wa Roma na kila mwamini, familia na jumuiya za kidini. Kwa mara nyingine tena janga la covid-19 limerudi katika mawazo ya Papa kwani amesema uwepo wao katika uwanja ni ishara ya kuanza kwa upya nchini Italia kipindi cha kushinda janga, japokuwa ametoa onyo kuwa wasiimbe ushindi kwa sababu bado inabakia ulazima wa kufuata sheria zilizowekwa. Kwa bahati mbaya, Papa Francisko amebainisha kuwa katika nchi nyingine virusi bado vinaendelea kuathiri watu wengi. Kwa kutoa mfano amesema, “siku ya Ijumaa iliyopita katika nchi amekufa mtu mmoja kila dakika moja, hii ni hali mbaya”. Kufuatia na hilo Papa Francisko amependa kuonyesha ukaribu wake kwa watu, wagonjwa na familia zao na wote ambao wanatoa huduma ya kuwatunza na kuwasadia.
Zaidi ya waathirika 400,000 wa covid-19
Ikiwa katika Nchi nyingi za Ulaya maambukizi yameanza kupungua, Bara la Amerika ya Kusini kuinyume chake idadi ya waathirika inazidi kupanda kwa kasi, kwa mujibu wa takwimu za wiki ya mwisho, idadi ya kati ya maambukizi mapya ya covid-19 imebainisha zaidi ya 100,000 kwa siku. Takwimu hizi zinathibitishwa ni jinsi gani janga bado halijamalizika! Maambukizi ulimwenguni kwa sasa ni milioni 6.9, waathirika ni zaidi ya 400,000 na Marekani ambao wanalipa gharama kubwa zaidi kwa vifo zaidi ya 109,000. Baada ya Uingereza kwa vifo zaidi ya 40,000, kuna sasa nchi ya Brazil ambayo tarehe 6 Juni 2020 imeonesha kuongezea kwa asilimia 904, na kufika vifo vya watu 35,930. Katika bara la Amerika ya Kusini wasiwasi mkubwa ni katika nchi ya Peru, ikipambana na upungufu mkubwa wa oksijeni. Kadhalika maambukizi yanaendelea katika Nchi za Mashariki na Afrika.
Janga la Covid -19 katika nchi za Amerika ya Kusini
Kufuatia na janga la virusi vya corona au covid-19, Kanisa la Chuquibambilla limeanza kugawa barakoa katika maeneo yaliyo hatari ya maambukizi. Hili ni eneo ambalo ni maskini sana nchini Peru, na shukrani kwa Shirika la Wamisionari wa Yesu Neno na dhabihu ambapo wamepata kutengeneza barakoa 2400 na kuwagaiwia wakazi wa maeneo hayo. Askofu Edison Farfán OSA, wa kwa kushirikiana na Caritas ya Chuquibambilla na Parokia ya San Salvador de Antabamba,wamejikita katika shughuli katika jumuiya mbalimbali za wakulima katika vijiji na miji ya wilaya za Antabamba, Cotabambas na Grau, Katika Mkowa wa Apurímac, ili waweze kupata hata msaada wa kiroho kwa upande wa Mapadre. Wamefanya kazi hili angalau vikapu 1, 200 vilivyojaa kila aina ya mahitaji viweze kusambazwa kwa familia zilizo athirika sana huko Chuquibambilla, kwa namna ya pekee katika wilaya ya Antabamba. Na hatimaye wameweka mpango wa kila parokia mahalia ili wasaidie watu walioambukiza na Covid-19.
Nchini Bolivia msaada kutoka Caritas kwa wafungwa wa Chonchocoro
Chakula na vifaa vya madawa vimetolewa na Caritas nchini Bolivia kwa wafungwa 490 katika Magereza ya Mtakatifu Pedro de Chonchocoro”, katika wakati huu wa janga la virusi vya corona. Jengo hilo lipo kwenye Plateau ya juu, zaidi ya mita 4 elfu juu ya usawa wa bahar. Nyumba ya gereza imezungukwa na nchi kavu, isiyo na maji ya kunywa ikiwa siyo tu yale ambayo hupatikana kutoka kisima kimoja na inazungukwa hewa ya baridi sana. Kwa njia hiyo, anasema Marcela Rabaza katibu mtendaji wa Caritas, kwamba “kuona misaada ya kibinadamu ikiwasili katika sehemu kama hiyo imezua hisia na shukrani miongoni mwa wafungwa”. Kwa hakika waliweza kupokea msaada huo na kutiwa moyo, tumaini na mwamko wa kutosahaulika na kwamba janga Covid-19 haliikuwakilisha kwao kama kikwazo cha kuweza kukutana nao.
Hata hivyo Caritas nchini Bolivia mwanzoni mwa Mei waliweza pia kuwafikia Gereza jingine la Villamontes, mahali ambamo wanaishi wafungwa 74 miongoni mwao kuna wazee na walemavu. Kituo hicho kilikabidhiwa vyakula, vifaa vya usafi na vifaa vya kusafisha, pamoja na vitu vingine kwa ajili ya utunzaji na uzuiaji wa Covid-19. Itakumbukwa kwamba michango hiyo ilifanywa shukrani kwa ufadhili kutoka Cafod,ambalo ni shirika la maendeleo la nje Katoliki la baraza la Maaskofu wa Uingereza na Wales.