Papa Francisko:Toeni kipaumbele hali halisi ya Siria!
Na Sr. Angela Rwezaula Vatican
Mara baada ya sala ya Malaika wa Bwana Papa Francisko akiwa katika Maktaba ya Jumba la Kitume tarehe 8 Machi 2020 katika Dominika ya Pili ya Kwaresima Papa Francisko amerudia kukumbuka vita nchini Siria na majanga ya kibinadamua ambayo baada ya miaka tisa bado yanaendelea kutesa watu hasa katika Kaskazini Magharibi mwa nchi nchi hiyo. Papa Francisko amewasalimia watu wote kwa namna ya pekee washiriki wa Mafunzo “walezi wa mtindo mpya ya mawasiliano” na waamini kutoka pande zote waliokuwapo katika uwanja wa Mtakatifu Petro.
Amewasalimia waamini na zaidi kikundi na makundi ambayo yanajikita katika jitihada za mshikamano kwa ajili ya watu wa Siria hasa kwa wakazi wa mji wa Idlib na Kaskazini magharibi wa Siria. “Niko nawatazama kutoka hapa mkilazimika kikimbia kutokana na kuongezeka kwa vita”. Amesema Papa. Aidha Papa Francisko amepyaisha wito wake kwa nguvu kutokana na uelewa wa uchungu mkubwa katika hali hiyo isiyo ya kibinadamu ambayo inasababaishawatu wengi kuteseka miongoni mwao wakiwemo watoto wanao hatarisha maisha yao. Papa anasema hawapawi kuondoa mtazamo mbele ya kipeo hiki cha kibinadamu, badala yake ni kutoa kupaumbele zaidi ya mambo mengine. Papa Francisko ameomba sana kusali kwa ajili ya watu wanaoteseka wa Kaskazini Magharibu mwa Siria na mji wa Idlib.
Ukaribu wa Papa kwa wenye maambukizi ya Corona na wahudumu. Papa Francisko ameonesha ukaribu wake kwa watu wanaoteseka na maambukizi ya sasa ya mafua ya virusi cya Corona na wale wote ambao wanashughulikia au kutoa huduma kwa ajili yao. Anaungana na ndugu maaskofu kuwatia moyo waamini wote ili waishi kipindi hiki kigumu kwa nguvu ya imani, uhakika wa matumaini na upendo wa hisani. Kipindi cha Kwaresima kitusaidie kuwapa watu wote maana ya kiinjili hata katika kipindi cha majaribu na uchungu, amesema Papa Francisko na kuhitimisha kwa kuwatikia mlo mwema na Dominika njema!