Papa Francisko:tusali kwa ajili ya Siria inayoteseka!
Na Sr. Angela Rwezaula –Vatican
Mara baada ya tafakari ametoa wito wa kuombea nchi ya Siria suala ambalo tayari alikuwa amekwisha sema mara baada ya Sala ya malaika wa Bwana Jumapili tarehe 9 Februari 2020. Katika siku hiyo Papa Francisko alikuwa amebainisha juu ya habari zenye kuwa na maumivu zinavyoendelea kufika kutoka kaskazini-magharibi mwa Siria, hasa kwa hali ya wanawake na watoto, ya watu waliolazimishwa kukimbia kutokana na kuongezeka kwa wanajeshi.
Papa akiwalekea hasa wahusika wa taasisi mbalimbali alisema: “Ninasasisha wito wangu kutoka moyoni kwa Jumuiya ya kimataifa na kwa wadau wote wanohusika ili kutumia vyombo vya kidiplomasia, majadiliano na mazungumzo, kwa kufuata Sheria ya Kimataifa ya Kibinadamu, ili kulinda maisha na hatima ya raia”. Kwa njia hiyp Papa Francisko aliomba waamini na mahujaji wote waliokusanyika kuomba kwa ajili ya nchi hiyo pendwa ya Siria inayosumbuka. " Salam Maria...."