Tafuta

Waamini wakisali sala ya Malaika wa Bwana na Papa Francisko tarehe 16 Februari 2020 Waamini wakisali sala ya Malaika wa Bwana na Papa Francisko tarehe 16 Februari 2020 

Papa Francisko:salam kwa mahujaji na waamini wote!

Dominika tarehe 16 Februari 2020,mara baada ya tafakari na sala ya Malaika wa Bwana,Papa Francisko amesalimia mahujaji wote walifika katika uwanja wa Mtakatifu Petro,Vatican.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Mara baada ya tafakari na sala ya Malaika wa Bwana, kwa mahujaji na waamini waliokusanyika katika uwanja wa Mtakatifu Petro Vatican, Jumapili tarehe 16 Februari 2020, Papa Francisko amewasalimia wote kwa namna ya pekee mahujaji kutoka Krotia na Serbia; Trappes, Ufaransa; Jimbo la Toledo, nchini Hispania; wanafunzi kutoka Taasisi ya Cuestablanca,  jijini Madrid.

Aidha amesalimia waamini wa Biancavilla, Fiuggi, Aprilia, Pescara na Treviso; Vijana waliopata kipaimara wa Serravalle Scrivia, Quarto  ya Altino na Rosolina.  Kwa wote amewatakia Dominka njema na kuwaomba kama kawaida yake ili kusali kwa ajili yake.

17 February 2020, 10:19