Papa Francisko:Lazima kutambua kudhibiti tamaa binafsi!
Na Sr. Angela rwezaula – Vatican
Injili ya leo kutoka Matayo 5,17-37, inajikita katika kuelezea juu ya hotuba za mlimani na kukabìliana na masuala ya utimilifu wa Sheria. Jinsi gani napaswa nitimize sheria, je nifanyeje. Ni kama Yesu anavyotaka kuwasaidia wasikilizaji wake kuhusu amri za Mungu zilizotolewa na Musa, akiwashauri kuwa na usikivu wa Mungu anayetufundisha kuwa na uhuru wa kweli na jukumu la Sheria. Ndiyo Mwanzo wa tafakari ya Papa ya Neno la Mungu, Dominika tarehe 16 Februari 2020 kwa mahujaji na waamini waliounganika katika uwanja wa Mtakatifu Petro kusali naye Sala ya Malaika wa Bwana.
Papa Francisko akiendelea na tafakari amesema, hii ina maana ya kuiishi kama zana ya uhuru. “Tusisahau hili yaani kuiishi Sheria kama zana ya uhuru inayonisaidia kuwa huru zaidi. Inayo nisaidia nisiwe mtumwa wa tamaa na dhambi". Papa Francisko amesema, "fikirieni vita na matokeo ya vita, fikirieni mtoto wa Siria aliyekufa juzi kwa sababu ya baridi, majanga mengi”. Yote hayo ni tunda la tamaa na watu wanaofanya vita na hawajuhi kudhibiti tamaa zao binafsi. Wanakosa kutimiza Sheria. Ikiwa ni kutawaliwa na vishawishi na tamaa huwezi kuwa bwana na kiongozi wa maisha binafsi, bali ni kukosa uwezo wa kutekeleza utashi na uwajibikaji.
Hotuba ya Yesu imegawanyika katika sehemu nne za ufafanuzi akisema “ mmesikia kwamba imenenwa; lakini mimi nawambia…”Misemo hii inataka kuelezea hali nyingi za maisha ya kila siku amesisitiza Papa na kuongeza kusema kwa mfano mauaji, uzinifu, talaka za ndoa na viapo. Yesu hatangui sheria zinazo tazama matatizo hayo bali anaelezea maana kamili na kuelekeza roho ambayo inatakiwa. Yeye anatoa sheria mpya ile inayotoka katika uchambuzi wa kawaida ili sheria kuwa na mtazamo ulio msingi wa kuweza kupokea Sheria katika moyo ambao ni kitovu cha nia, cha maamuzi, cha maneno na ishara za kila mmoja wetu.
Kutoka moyoni ndimo chanzo cha matendo mema na yale mabaya. Kwa kupokea Sheria ya Mungu katika moyo ndiyo kutambua kuwa usipompenda jirani ni kama kujiua binafsi kwa namna fulani na wengine kwa sababu chuki, upendeleo na migawanyiko vinaua upendo wa kidugu ambao ni msingi wa uhusiano wote wa kibinafsi. Hii ni sawa sawa, Papa francisko anabainisha kwa kile ambacho amesema juu ya vita masengenyo kwa maana mdomo unaua. Kwa kupokea Sheria ya Mungu ndani ya moyo ni kutambua kuwa tamaa zinapaswa zidhibitiwe, kwa maana si kila kitu kinachotamaniwa unaweza kuwa nacho na siyo vema kungukia kwenye hisia za ubinafsi na kutawaliwa na tamaa. Sheria ya mungu inapopokelewa kutoka moyoni ni kuelewa kwa kuna ulazima wa kuachana na mtindo wa maisha ya kutoa ahadi bila kutimiza na kama pia kuachana na tabia za kuapa uongo na kuweza kuwa na uamuzi wa kutokuapa kabisa ili kuweza kuchukua jukumu la tabia kamili ya kuwa mkweli kwa wote.
Papa Francisko aidha amesema kwamba “Yesu anatambua vema jinsi ambavyo siyo rahisi kuishi Amri za Mungu na kwa mtindo huo kwa ujumla. Kwa njia hiyo anatupatia msaada wake wa upendo. Yeye alikuja duniani si kwa ajili ya kutoa maisha na utimilifu wa Sheria tu, bali Yeye alikuja kutupatia neema yake na ili sisi tuweze kufanya mapenzi ya Mungu, kwa kumpenda Yeye na ndugu. Yote yanawezekana kwa Neema ya Mungu! Na zaidi utakatifu siyo jambo jingine zaidi ya kutunza zawadi hii ya neema ya bure tuliyopewa na Mungu. Hii inatakiwa kukabidhi kwake Yeye, katika neema yake, katika zawadi yake ya bure ambayo ametujalia na kuipokea kwa mikono ambayo yeye mwenyewe anatusibiri daima ili jitihada zetu, ulazima wetu wa jitihada uwezekane kusaidiwa kwa msaada wake na pia kutulizwa na wema na huruma.
Yesu leo hii anataka tuendelee katika njia ya upendo ambao alituelekeza kwa moyo. Hii ndiyo njia ya kufuata ili kuishi kama wakristo. Bikira Maria atusaidiè kufuata njia iliyopitiwa na Mwanae ili kufikia furaha ya kweli na kueneza kila mahali haki na amani, amehitimisha Papa Francisko tafakari yake .