Papa amekutana na wajumbe wa Chama cha Mfuko wa Galileo katika mapambano dhidi ya biashara ya binadamu na amezindua "super nuns" kwa ajili ya ukosanyi fedha kusaidia waathirika Papa amekutana na wajumbe wa Chama cha Mfuko wa Galileo katika mapambano dhidi ya biashara ya binadamu na amezindua "super nuns" kwa ajili ya ukosanyi fedha kusaidia waathirika 

Papa amezindua “Super Nuns” kusaidia watawa dhidi ya biashara ya utumwa!

Katika fursa ya Siku ya Maombi na tafakari kuhusu mapambano dhidi ya biashara ya binadamu na utumwa,kwenye Maktaba ya Nyumba ya Kitume Vatican, Papa Francisko amekutana kwa faragha na baadhi ya wajumbe wa Mtandao wa Talita Kum na Mfuko wa Chama cha Galileo ili kuzindua Jumuiya ya “Super Nuns” mtandao unaokusudia kukusanya fedha kwa ajili ya watawa wanaohusika katika kuwaokoa waathirika wa biashara ya wanadamu na watumwa.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Kwa  bofya la kwanza, Papa Francisko amezindua jukwaa hili la  “Super Nuns”, ambalo ni jukwaa la Patreon lililobuniwa kwa ajili ya kukusanya fedha kwa ajili ya waathirika wa biashara haramu ya binadamu na kufadhili miradi ya utunzaji na msaada kwa upande wa watawa wote wanaojikita na shughuli hii ya kusaidia waathirika.

Mradi uliozinduliwa na Talitha Kum ambao ni Mtandao wa Kimataifa  wa Kitawa unajikita katika kujenga maisha  ya watu, wakati huo wakiwalinda dhidi ya wanafanya biashara haramu na uliofadhiliwa na Mfuko wa chama cha Galileo  ambao hutoa ushirikiano kwa wadau mbali  mbali kutoka kwa wasanii tofauti wa michoro ya barababarni mmojawapo akiwa ni  Stephen Power, wa Amerika  kwa usanii wake wa  ESPO. Huyu ni  msanii wa kuchora michoro mbali mbali mikubwa barabarani, na Leiji Matsumoto, maarufu wa michoro wa Kijapani.

Mara kadhaa  Papa amewasha na kutazama juu ya janga hili la biashara ya watu na kuomba viwepo vitendo halisi.  Katika tukio hili Papa  amesalimiana na kila mtu binafsi na na Sr. Gabriella Bottani, mratibu wa kimataifa wa Talitha Kum, ambaye ameeleza juu ya kuanzishwa wa tovuti hii . Msanii Stephen Power alimemwomba Papa atie sahihi yake katika  nakala ya picha ya kwanza na moja amepewa Papa  Francisko mwenyewe.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na watawa  wengine wa Talitha Kum, walioanzisha  kwa mpango wa Jumuiya ya Kimataifa ya wa Mama Wakuu  wa mashirika ya Kitawa (UISG) na kwa miaka 10 pia amekuwa wakikuza ushirikiano na kubadilishana habari kati ya wanawake na wanaume waliowekwa wakfu katika nchi 70 ulimwengu ili kuweza kupambana na  kuondoa kabisa janga la utumwa.

08 February 2020, 15:24