Umuhimu ya kiekumene una uwezo wa kuzaa zawadi nyingine za kiroho, na hivuyo ni mwaliko wa kufanya kazi kwa ajili kuonyeha kuwa kila mtu ni mwenye thamani machoni pa Mungu. Umuhimu ya kiekumene una uwezo wa kuzaa zawadi nyingine za kiroho, na hivuyo ni mwaliko wa kufanya kazi kwa ajili kuonyeha kuwa kila mtu ni mwenye thamani machoni pa Mungu. 

Papa Francisko:uwajibu wa ukarimu kwa wageni ni upendo kama wa Mungu!

Akikumbuka Wiki ya kuombea umoja wa wakristo Papa Francisko katika tafakari ya Katekesi yake amejikita juu ya safari ya Mtakatifu Paulo wakati wa kufika kisiwa cha Malta na ukarimu aliotendewa na wanyeji ambao anasema ni fadhila muhimu ya kiekumene,yenye uwezo wa kuzaa zawadi nyingine za kiroho.Anatoa mwaliko wa kufanya kazi kwa ajili kuonyesha kuwa kila mtu ana thamani machoni pa Mungu.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Papa Francisko katika katekesi yake yak ila Jumatano kwa waamini na mahijaji wote waliungunika katika ukumbu wa Paulo VI mjini Vatican tarehe 22 Januari 2020 ameanza kusema kuwa Kateksi ya lei inajikita ndani ya Wiki ya Kuombea umoja wa Wakristo. Mada iliyo chaguliwa mwaka huu ni ile ya ukarimu na ambayo imeweza kufafanuliwa kwa mapana katika jumuiya ya Malta na Goo kuanzia katika hatua ya Matendo ya Mitume ambayo inasimulia juu ya ukarimu uliotolewa na wakazi wa Malta kwa Mtakatifu Paulo na wenzake walionusurika akiwa nao. Kwa dhati katika tukio hilo Papa Francisko amethibitisha kuwa alijikita nalo katika katekesi ya wiki mbili zilizopita.

Uzoefu wa janga la kunusurika

Papa Francisko akianza na uzoefu wa janga wa kushangaza hasa la kunusirika kwa meli waliyo safiri nayo  Paulo  na wenzake ilikuwa kweli hatarini. Na hii ni kwa sababu Meli waliyokuwa wanasafiiri ilikuwa na vitu vingi. Kwa siku kumi na nne walikuwa baharini, ambapo liwe jua au nyota vilikuwa havionekani, na kwa maana hiyo wasafiri walihisi mfadhaiko, na wamepotea. Chini yao, bahari inazunguka kwa  vurugu dhidi ya meli na wanaogopa kwamba itavunjika kutokana na  nguvu ya mawimbi. Kutoka juu wanapigwa na upepo na mvua. Nguvu ya bahari na dhoruba ina nguvu sana na haijali hatima ya mabaharia na kulikuwa na zaidi ya watu 260! Lakini Paulo anayetambua kuwa siyo hivyo anaamu kuzungumza. Imani yake inamfanya atambua kuwa maisha yake yako mikononi mwa Mungu na kwamba Yesu aliyefufuka katika wafu alimwita Yeye Paulo apeleke Injili hadi miisho ya dunia. Imani yake inamwaminisha kwa Mungu na kwa upande wa Yesu aliye mwonesha ni Baba wa upendo. Kwa maana hiyo Paulo anawambia wenzake kuwa safari hiyo ni ya imani  na anawatangazia kuwa Mungu hataruhusu hata unywele mmoja vichwani mwao upotee.

Unabii wa Yesu unajionesha katika kisiwa cha Malta

Unabii huo ulijionesha tu wakati Meli iliposimama katika mwambao wa Kisiwa cha Malta na wasafiri wote waliweza kufika sala salimini katika nchi kavu. Hapo waliweza kufanya uzoefu wa jambo jipya.  Tofauti na vurugu za kikatili za bahari ya dhoruba, wanapata ushuhuda wa “ubinadamu ulio adimu” wa wenyeji wa kisiwa hicho, amesisitza Papa. Watu hawa, kwa upande wao ni wageni kwao, wanazingatia na kuwa makini kwa mahitaji yao. Waliweza kuwaashia moto ili wapate jotyo, waliwapatia chakula na makazi ili kutoka kwenye  mvua.

Hata kama walikuwa hawajapata Habari Njema ya Kristo, walionesha upendo wa Mungu kwa matendo ya dhati na ukarimu. Na kiukweli, ukarimu wa hiari na ishara zinaonyesha kitu cha upendo wa Mungu. Na ukarimu wa wenyeji wa kisiwa cha Malta ulilipwa na miujiza ya uponyaji ambayo Mungu analifanya kazi yake  kupitia kwa  Paulo kwenye kisiwa hicho. Kwa hivyo, ikiwa watu wa Malta walipewa ishara kubwa ya utoaji wa upendo mkuu  kutoka kwa Mungu kupitia kwa Mtume, hata yeye pia kwao alikuwa shuhuda wa upendo wa huruma ya Mungu, Papa Francisko amesema.

Umuhimu wa fadhila za kiekuemene

Papa Francisko akiendelea kufafanua  amekazia kuwa ukarimu ni muhimu na zaidi ni muhimu wa fadhila za kiekumene. Awali ya yote maana ni  kutambua kuwa wakristo wengine ni ndugu wa kweli, kaka na dada katika Kristo. Sisi sote ni ndugu. Hata hivyo Papa anatoa mfano kwamba: mwingine inawezakana kusema: “ huyo ni mprotestanti, hutìyo ni muorthodox…. Haijalishi kwa maana, sisi sote ni ndugu katika Kristo”. Na siyo tendo la ukarimu wa njia moja tu, kwa sababu tunapowakaribisha Wakristo wengine tunawakaribisha kama zawadi ambayo tumepewa. Kama  ilivyokuwa kwa wenyeji wa Malta, kwa hakika ni watu wema amekazia kusema Papa.., na zaidi tunalipwa, kwa sababu tunapokea kile ambacho  Roho Mtakatifu amepanda katika kaka  na dada zetu, na hii inakuwa zawadi hata sisi pia, kwa sababu Roho Mtakatifu pia hupanda neema  zake kila mahali.

Kukaribisha watu wa tamaduni nyingi ni kuonesha upendo wa Mungu

Kukaribisha wakristo wa tamaduni nyingine maana yake ni kuonesha upendo wa Mungu alio nao kwao na hivyo kwa sababu ni wana wa Mungu na ndugu zetu na zaidi maana  ni kukaribisha kile ambacho Mungu alitimiza katika maisha yao. Ukarimu wa kiekumene utahitaji utayari wa kusikiliza wakristo wengine, kuwa makini katika historia binafsi za imani yao na katika historia yao ya kijumuiya, jumuiya ya imani na utamaduni tofauti na wa kwetu. Ukarimu wa kiekumene unapelekea shauku ya kutambua uzoefu ambao wakristo wengine wanafanya kwa Mungu na kusubiri kupokea zawadi ya kiroho itokanayo na ukarimu huo. “Hii ni neema na  kugundua”, anasema papa na kurudia kuwa  “hiyo ni neema”. Papa Francisko amekumbuka  nyakati zilizopita katika nchi yake na kutoa mfano kuwa: “walipokuwa wanakuja baadhi ya wamisionari wa kiinjili, makundi ya wakatoliki walikuwa wanakwenda kuchoma mahema yao. Hii siyo ukristo. Kwa sisi sote ndugu na kama ni ndugu tunapaswa kukarimu mmoja na mwingine”.

Leo hii mahali ambapo Paulo alipitia na kunusurika bado kuna hatari ile ile

Leo hii baharini mahali ambapo Paulo alinusurika na wenzake, bado kwa mara nyingine  tena ni mahali pa hatari ya maisha ya wasafiri tena.  Duniani kote wanaume na wanawake wahamiaji wanakabiliana na safari ya hatari wakikimbia vurugu, wakikimbia vita na kukimbia umasikini. Kama Paulo na wenzake wanafanya uzoefu wa sintofahamu, ugumu wa jangwa, mito na bahari… na mara nyingi hawaruhusiwi kupita bandarini, Papa Francisko ameeleza wazi. Na zaidi amezidi kusema : “Lakini kwa bahati mbaya mara nyingi wanakutana na ugumu na  na uadui mbaya zaidi wa watu”. Leo hii wananyanyaswa na wafanyabiashar haramu!. Leo hii wanatendewa kama idadi na kama tishio na baadhi ya  watawala wengine! Wakati mwingine wanakosa ukarimu na kuwakataa na kuwatupa kama wimbi katika umaskini au hatari ambayo wameikimbia.

Wakristo lazima tufanye kazi kwa pamoja kuonesha wahamiaji upendo wa Mungu

Sisi, kama Wakristo, lazima tufanye kazi kwa pamoja ili kuwaonyesha wahamiaji upendo wa Mungu uliofunuliwa na Yesu Kristo. Tunaweza na tunapaswa kushuhudia kwamba siyo tu kuwapo uadui na kutojali, bali kwamba kila mtu ni ni mwenye thamani kwa Mungu na anapendwa naye. Mgawanyiko ambao bado upo kati yetu unatuzuia kuwa ishara kamili ya upendo wa Mungu. Inatakiwa kufanya kazi pamoja, ili kuishi ukarimu wa kiekuemene, hasa kwa wale ambao maisha yao yako  hatarini zaidi, nazidi hali hii itatufanya sisi sote kuwa  Wakristo  hai  ikiwa ni Waprotestanti, waorthodox, Wakatoliki, yaani Wakristo wote, kuwa wanadamu bora, wanafunzi bora na watu wakristo walio na umoja wa Kikristo. Hii itatuleta pamoja  karibu karibu na umoja, ambao ndiyo mapenzi ya Mungu kwetu.

22 January 2020, 12:48