Papa akumbuka siku ya maangamizi makubwa ya Auschwitz!
Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican
Mara baada ya Tafakari ya Neno na Sala ya Malaika wa Bwana, Papa Francisko amekumbusha juu ya maadhimisho ya kumbu kumbu ya miaka 75 tangu kukumbolewa kwa kambi ya maangamizi makuu ya huko Auschwitz-Birkenau, ambayo imekuwa ishara ya mahuaji ya kiyahudi. Mbele ya janga hili lisilo la kibinadamu, amesema Papa “hazikubaliki zile sintofahamu, hivyo ni muhimu kufanya kumbu kumbu na tarehe 27 Januari kila mmoja anakumbushwa kusali kwa hilo akipinga suala hili lisirudiwe tena”. amesema Papa.
Kujifungulia katika huruma ya Baba
Papa Francisko akikumbusha juu ya Dominika ya Kwanza ya Neno la Mungu kwa mahujaji na waamini wote waliokusanyika katika uwanja wa Mtakatifu Petro Vatican tarehe 26 Januari 2020 wakati wa tafakari yake kabla ya sala ya Malaika wa Bwana, amejikita juu ya Injili ya siku ya ya Jumapili ambayo ilikuwa inajikita juu ya kuanza kwa Utume Yesu kwa watu wote. Alianzia Galilaya katika eneo la pembezoni, ukilinganisha na Yerusalemu, na ambalo lilikuwa linatazama vibaya kutokana na mchanganyiko wa wapagani, lakini Yesu alianzia hapo kuhubir na kutangaza maneno haya: “Tubuni kwa kuwa Ufalme wa Mbingu unakaribia”
Mahubiri hayo Papa Francisko amebainisha kuwa ni kama yenye nguvu ya mwanga ambao inapitia katika giza. Kuja kwa Yesu ambaye ni mwanga wa ulimwengu, Mungu Baba amejionesha ubinadamu wake wa ukaribu na urafiki, uliotolewa bure, licha ya kwamba sisi kutostahili. Na hizi ndizo zawadi za kutunza anaeleza Papa Francisko. Mara nyingi inajionesha kuwa na ugumu wa kubadili maisha, kuacha njia za ubinafsi, za ubaya, kuacha njia za dhambi kwa sababu zinajikita katika mchakato wa uongofu binafsi tu na kwa njia ya nguvu binafsi na siyo kwa katika njia ya Kristo na Roho. Lakini kumfuasa Bwana, hakuishii katika nguvu binafsi, hapana. kwa kuamini hilo Papa ameongeza kusema, inaweza ikawa hata dhambi ya ukiburi. Kumfuasa Bwana hakuwezi kuishia na nguvu binafsi , badala yake lazima ufafanuiliwe kwa njia ya ufunguzi wazi katika imani ya moyo na katika akili ya kupokea Habari Njema ya Yesu. Hili ndilo Neno la Yesu, Habari Njema ya Yesu, yaani Injili ambayo inabadili ulimwengu na mioyo! Sisi tunaitwa zaidi kuamini Neno la Kristo na kujifungulia katika huruma ya Bwana na kuacha tubaidilishwa kwa neema ya Roho Mtakatifu.
Kutangaza uhuru wa kweli
Kwa kufanya hivyo Papa Francisko anakumbusha kuwa, ndiyo kuanza mchakato wa kweli wa uongofu. Na ndiyo sawa na ilivyo watokea mitume wa kwanza. Mkutano na Mungu yaani mwalimu, kwa mtazamo wake, kwa neno lake, aliwapa msukumo wa kumfuata na kubadili maisha kwa kijikita kwa dhati katika huduma ya Ufalme wa Mungu
Kufuata nyayo za Mwokozi
Watu wote Papa Francisko anahitimisha, wanaalikwa kuwa wajumbe wa Neno la Mungu: “Kukutana kuna shangaza hajabu na ni uamuzi wa kweli na Yesu ambao ulitoa mwanzo wa wafuasi kutembea, kuwabadili na kuwa watangazaji na mashuhuda wa upendo wa Mungu kwa watu wake. Kuiga mifano ya wajumbe hao wa shauku kubwa ya Neno la Mungu , kila mmoja anaweza kweli kuanza hatua moja ili kuelekea katika nyayo za Mwokozi na hatimaye kuwapa matumaini wenye kiu”.
Siku ya ugonjwa wa Ukoma
Papa Francisko amekumbusha pia kwamba: “ leo inaadhimishwa Siku ya ugonjwa wa Ukoma Ulimwenguni” Tuko karibu na watu wote waliathiriwa na dalili hizi za Hansen na wale wote kwa namna nyingine wanaowasadia wagonjwa hao”. Mwaka huu umefikia toleo la 67 na ambalo linabeba kauli mbiu: "Usiwepo kamwe ukosefu wa haki, ubaguzi, ukoma ulimwenguni".
Ukaribu wa wagonjwa kwa mlipuko wa virus uliosambaa nchini China
Papa Francisko katika kuendelea amekumbusha hata ukaribu na watu wagonjwa kwa sabau ya virusi ambavyo vimesambaa nchini China.” Ee Bwana uwapokee marehemu katika amani yako, uwafariji familia na kuwasaidia katika jitihada za Jumuiya ya nchi ya China ambao wanaendelea kupambana na mlipuko huo”
Vijana wa Chama Katoliki
Papa Francisko amesalimia vijana wengi wasichana na wavulana wa Chama katoliki nchini Italia walitoka katika maparokia na shule katoliki za Jimbo la Roma, anasema wamefika wakiwa katika msafara wa amani. Watoto wawili wameweza kusoma ujumbe wao wakiwakilisha vijana wote na baadaye wakatupa mapuzo juu yenye rangi nyeupe na njano. Katika ujumbe wao wanasema, wamefika hapo kwa ajili ya kupaza sauti ya kutaka amani katika mji wao na katika dunia nzima. Wamekuja katika Dominika ya kwanza ya Neno la Mungu ili watu wote waweze kujika katika usikivu wa thamani ya Neno la Mungu linalobeba nafasi kubwa ya maisha ya kila mtu. Na mwaka huu kwa upande wao utakuwa ni kwa ajili ya mambo makuu na matarajio yao ya furaha.