Papa Francisko:heri ya mwaka mpya kwa nchi za mashariki!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Salam na heri na wito wa pamoja katika kusali na kuomba zawadi ya amani, majadiliano na mshikamano ni mambo yaliyotajwa na Papa Francisko mara baada ya katekesi yake kwa mahujaji na waamini waliofikia katika ukumbi wa Paulo VI, Vatican, akiwalenga yale makanisa na nchi ambazo wanaadhimisha Mwaka mpya tarehe 25 Januari 2020 hasa katika nchi za mashariki na nyingine zenye kalenda ya kutumia mwezi.
Aidha Papa Francisko anakumbuka familia
Kadhalika Papa Francisko amekumbuka familia zote ili ndani mwake paweza kuwa mahali ambao kunaoneshwa na kufundishwa na mfano wa elimu na fadhila ya ukarimu na hekima, heshima kwa ajili ya kila mtu na maelewano ya kazi ya uumbaji. Anaomba Mungu aweze kutoa zawadi ya lazima katika dunia ya leo. Hakusahau kama kawaida yake kuwasalimia mahujaji wote kutoka pande zote za dunia, wakiwemo vijana, wazee, wagonjwa na wanandoa wapya.