Nia za sala ya Papa Januari 2020:kuhamasisha amani na haki duniani!
Na Angela Rwezaula – Vatican
Kukaribisha, kushirikishana na kuhamasisha ndiyo mambo matatu ambayo Papa Francisko yanajikita komba katika sala moja. Ni kutaka kupata amani na haki katika dunia ambayo imejaa migogoro na yenye ukosefu wa maelewano. Na kila ombi Papa Francisko anafafanua ni kwa jinsi gani inapaswa isindikizwe na jitihada za kila mmoja.
Katika Nia za maombi ya Papa Francisko kwa mwezi Januari 2020 zinasema: “Katika dunia ambayo imegawanyika na kupasuka, ninataka kuwaalika kwenye upatanisho na udugu kati ya watu wote waamini, hata kati ya watu wenye mapenzi mema. Imani yetu inatupelekea kueneza thamani za amani na kuishi pamoja na wema wa pamoja. Tusali ili wakristo na wale wa madhehebu mengine na watu wenye mapenzi mema waweze kuhamasisha kwa pamoja amani na haki duniani. Asante”
Mchango wa kila mtu
Ili kuwelewa anafafanua, inatosha kurudi nyuma ya miezi iliyopita, kuona umuhimu wa uhai wa Papa anaoutoa mchango huo wakati machoni pake akiwaunganisha kila mtu katika mchakato wa mariadhiano, haki na amani kati ya watu na kati ya mataifa. Mfano huo ulionekana huko Tokyo, tarehe 25 Novemba 2019 akiwa amesimama katika Jumba Kuu la Kantei, jumba linalojumuisha hata maofisi na makazi ya Waziri Mkuu wa Japan, mbele ya viongozi wa mamlaka ya nchi na wa kidiplomasia, ambapo Papa Francisko katika hotuba yake alisema: “Historia inatufundisha kuwa migogoro kati ya watu na mataifa hata ile mikubwa inaweza kupata muafaka muhimu kwa njia ya majadiliano, ambayo nimoja ya silaha tosha ya mwanadamu na yenye uwezo wa kuhakikisha amani ya kudumu”. Huo ulikuwa ni ujumbe wa hotuba yenye nguvu ambayo inaojikita katika misingi mikuu ya Papa tangu aanze utume wake na mbaye hadi sasa anaendelea, hachoki kutoa mialiko kwa wote ili wawe wajenzi wa kweli wa amani.
Udugu dhidi ya mauaji
Vile vile katika kuendeleza kuona thamani ya amani, Papa Francisko anakumbusha hata katika Ujumbe wake 53 wa Kuombea amani duniani kwa mwaka 2020 huku akikumbusha kwa dhati kwamba “amani ni tunu yenye thamani, na kitu cha tumaini letu, ambacho wanadamu wote tunaomba”. “Ushuhuda mbaya wa mizozo ya wenyewe kwa wenyewe na ya kimataifa, ambayo mara nyingi huchukiza na kufanya vurugu bila huruma yoyote, imeweka alama kwa muda mrefu katika mwili na roho ya kibinadamu”. Na zaidi kwa hakika anasema, “kila vita inaonesha mauaji ambayo yanaharibu mpango wa udugu uliowekwa muhuri katika wito wa familia ya kibinadamu”.
Mtandao wa nia ya maombi ya Papa
Ikumbukwe kwamba Nia za Papa zinasambazwa na Mtandao wa Utume wa Sala Kimataifa. Mtandao huu uliundwa nchini Ufaransa kwa mara ya kwanza kunako tarehe 3 Desemba 1844 na padre mmoja mjesuiti aliyekuwa anaitwa Francesco Saverio Gautrelet. Mwaka 2019, mtandoa huo umetimiza miaka 175 tangu kuzaliwa kwak japokuwa umepata kuridhiwa na Papa Francisko kunako mwaka 2014. Tangu mwanzo wa miaka ya 1900 ulikuwa na wafuasi zaidi ya milioni 13, lakini hadi sasa namba imezidi kuongezeka na kufikia tayari milioni 35 katika kila kona ya sayari hii.