Timu ya Taifa Italia:ipo thamani ya mpira wa vitambaa chakavu!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Baba Mtakatifu Francisko amekutana na kusalimiana na kikundi cha Timu ya Taifa ya wanamichezo wa mpira wa miguu nchini Italia, tarehe 13 Oktoba 2019, kabla ya kuanza maadhimisho ya Misa Takatifu kwa ajili ya kuwatangaza watakatifu wa 5 wapya wa Kanisa. Akizungumza nao amewashukuru kumtembelea hasa ujasiri wao mara baada ya mchezo wao Jumamosi 12 Oktoba katika uwanja wa Mpira mjini Roma wakipambana na Timu ya mpira kutoka nchini Ugiriki na wakashinda kwa mabao 2 kwa bila. Baba Mtakatifu amesema wamefika kwa haraka wakiwa wanaonekana na roho ya ibada. Aidha ameeleza kwa jinsi gani kabla wametembelea watoto katika Hospitali ya Bambin Gesù, ambapo pale wamewezeza kuonesha upendo wa kila mmoja ambao mara nyingi unafichika ndani mwao, lakini mbele ya watoto daima unajitokeza nje.
Baba Mtakatifu amebainisha kuwa wakati anaingia katika ukumbi kushoto kwake ameona mchoro wa ubunifu unaohusu kazi ya uumbaji wa dunia. Na hivyo amewashauri watakaopoondoka wautazame kwa upya. Akiataka kuelezea mchoro huo amesema ni mikono ya Mungu ambayo inafanya kuzaliwa mtoto. Msanii wakati wa kuchora alifikiri kila mtoto anayezaliwa kwamba ni kazi ya uumbaji. Daima ni uumbaji hata wakati mwingine kiumbe anapokuwa na itilifu, kuna uchungu wa watoto, na kama wao walivyo fanya uzoefu wa ziara hiyo kwa watoto, pia wanafahamu hata wengine, jinsi ilivyo mara nyingi msalaba wa familia. Lakini yote hayo ni mikono ya huruma, anasisitiza Baba Mtakatifu Francisko. Watoto wanaelewa lugha na kuwa na karibu daima kwa njia ya huruma itumikayo. Ni lugha ya upendotu ambayo mtoto anaweza kuelewa. “Ninatambua jinsi mlivyokuwa nao. Ninawashukuru kwa ishara hiyo ya upendo. Asante”
Baba Mtakatifu aidha amegusia juu ya zawadi waliyo wapatia watoto hao. Zawadi hiyo ni mpira na kwamba, wamewapatia jambo zuri sana, ameongeza kusema kwa kutoa mfano kuwa hata Mtakatifu Don Bosco alikuwa anasema hivyo! jinsi gani ya kuwafanya watoto wawe na furaha, kwa jinsi gani ya kuwakusanya watoto? Nyakati zile katika mtaa wa kimasikini na uliobaguliwa, alitupa mpira barabarani na mara watoto walikusanyika”. Mpira una kivutio. Baba Mtakatifu Francisko akiendelea na hisotria hii kuhusu mpira amekumbuka kuwa, kulikuwa na kiwanja kidogo sana, mita chache karibu na nyumbani kwao. Pale walikuwa wanacheza japokuwa si wakati wote walikuwa na mpira kwa sababu wakati ule mpira ulikuwa wa ngozi na ulikuwa ni gharama. Hapakuwapo bado na plastiki na ile ya mipira haikuwapo… kulikuwapo na mipira ya vitambaa chakavu. Hata kwa njia ya mpira wa vitambaa chakavu unafanya miujiza. Aidha amekumbua kwamba,“mtoto mmoja nchini Msumbiji nikiwa katika ziara aliniletea mpira wa vitambaa chakavu. Ndiyo ndiyo mpira tuliokuwa tunacheza hivyo. Ni muhimu kuwa na mpira pale na pale wao wanacheza ndani yake.
Baba Mtakatifu Francisko akiendelea na mazungumzo yake na wachezaji wa Timu ya Kitaifa ya mpira wa miguu amesema, kuna filamu moja ya Argentina yenye kichwa “Pelota de trapo”, yaani “ mpira wa vitambaa chakavu, ambao unafanya kuona roho ya ajabu na kama alivyofafanua haya Rais wao (FIGC) kuwa “hata kwa njia ya mpira wa vitambaa chakavu”. Filamu iliyotengenzwa kwa miaka ya 40 ilikuwa nzuri sana na ya kimashairi. Baba Mtatifu akihitimisha amewaachia kazi mbili ya kisanaa ya kutafakari kwa kina, kwamba ya mchoro kuhusu huruma ya Mungu katika uumbaji wa kila mtu na ya mtoto; pili ile inayohusu mpira wa kitambaa chakavu katika filamu. Labda wao wanaweza kupendelea kuitazama, amesbainisha. Kadhalika amewashukuru sana tena kwa ishara hiyo ya watu wakubwa na wenye uwezo wa kuwa na huruma na kukaribia watoto. Na labda mmoja wapo kati yao , ameweza kulia. Huruma ya Mungu haisaliti kamwe! Mtu anafanya ishara ya huruma na baadaye anajificha na kulia kwa sababu ndiyo hivyo! Maisha ndiyo hivyo. Na ndiyo ishara zinazofanya vizuri maisha na ndizo ishara zinazopelekea kuleta afya bora!