Sinodi ya kutafuta njia mpya za uinjilishaji na uhamasishaji!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Baba Mtakatifu Francisko kabla ya Sala ya Malaika wa Bwana Jumapili tarehe 6 Oktoba 2019 kwa waamini waliounganika katika uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican amekumbusha kuwa muda mfupi katika Kanisa Kuu la Mtatifu Petro wamefanya maadhimisho ya Ekaristo ikiwa ndiyo mwanzo wa ufunguzi wa Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya Kanisa la Amazonia. Kwa wiki tatu anasema, Mababa wa Sinodi wanataungana pamoja na mfuasi wa mtume Petro ili kutafakari juu ya utume wa Kanisa la Kanda ya Amazonia, juu ya uinjilishaji na juu ya uhamasishaji wa ekolojia fungamani.
Maombi ya waamini kwa ajili ya Sinodi ya Maaskofu
Baba Mtakatifu Francisko kufuatia na tukio hilo la Sinodi ya Maaskofu, anawaomba waamini wote ili kuwasindikiza kwa sala katika tukio hili la Kanisa na ili waweza kweli kuishi muungano wa kindugu huku wakiongozwa na maongozi ya Roho Mtakatifu na ambaye daima awaoneshe njia kwa ajili ya kushuhudia Injili.
Shukrani kwa mahujaji toka pande za dunia
Aidha Baba Mtakatifu Francisko amewashukuru mahujaji wote waliofika kutoka Italia na sehemu mbali mbali za dunia. Akiwataja baadhi waamini kutoka Heidelberg, Ujerumani , Poland, wanafunzi kutoka Ujerumani na wengine kutoka Argentina. Amekumbuka mahujaji kutoka Castelli Romani waliofanya matembezi mshikamani wa amani kama vile hata wale wa Camisano Vicentino. Na kwa wote wanawatakia Dominika njema na kuwaomba kama kawaida yake wasisahu kusali kwa ajili yake.