Sala ili kusikiliza kilio na kutafuta suluhisho nchini Iraq
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya katekesi yake tarehe 30 Oktoba 2019 kwa waamini na mahuji kwenye kiwanja cha mtakatifu Petro, amewasalimia wote na kutoa wito mkubwak ufuatia na hali halisi ya ghasia na vurugu zinzaoendelea ulimwenguni na kwa namna ya pekee nchini Iraq. Anawaombea watu wote ili waweze kuwa na maisha yenye hadhi na utulivu, majadiliano na upatanisho na haki ya kutafuta suluhisho ili kufikia amani na msimamo wa nchi ya Iraq nzima.
Maandamano ya kupinga ufisadi
Baba Mtakatifu Francisko akifikiria nchi hii ya Iraq na ambayo kwa sasa unaendelea na maandamanotangu mwanzoni mwa Mwei Oktoba kwa ajili ya kupinga hali halisi ya ifisadi na ukosefu wa ajira, anaomba hali hii imeweze kuisha, kwa maana ghasia hizi zimekwisha sababisha vifo vingi na majeruhi. Hadi sasa ni zaidi ya waandamanaji 250 waliouwawa huko Baghdad na katika miji ya Kusini mwa nchi.
Watu wa Iraq wasaidie Jumuiya ya Kimataifa
Kutokana na hiyo Baba Mtakatifu Francisko anatoa salam za rambi rambi kwa wanafamilia na waathrika wote majeruhi na kuonesha ukaribu wake. Na wakati huo huo anawaalika mamlaka ya nchi kusikiliza kilio cha watu ambao wanapaza sauti wakiomba maisha yenye hadhi na utulivu. Anawashauri watu wote wa Iraq wajikite kusaidia haya Jumuiya ya kimataifa katika kufuata njia ya majadiliano na upatinisho wakati wanatafuta suluhisho la haki katika changamoto na matatizo ya nchi. Anawaombea watu wote wanaoteseka ili waweze kupata amani na msimamo wa nchi baada ya miaka mingi ya vita, vurugu na kuteseka sana.