Wito wa Papa kwa ajili ya Camerun:Lazima kutafuta suluhisho la amani ya kudumu!
Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican
Baba Mtakatifu Francisko wakati wa salam zake kwa wote waliodhuria ibada hiyo mara baada ya kumaliza misa Takatifu amesema kuwa wamepyaisha nia za Kanisa na kwa ajili ya kila aina ya watu waathirika katika mzungumko. Aidha amesema kwa kuungana na waamini wa majimbo yote ulimwenguni ambao wanaadhimisha Siku ya Wahamiaji na Wakimbizi duniani, wanathibitisha hata ulazima kwamba pasiwepo jamii yoyote nyumba awe mzalendo tayari wa siku nyingi au aliye mgeni.
Sanamu kubwa katika uwanja wa Mtakatifu Petro
Katika kusisitiza jitihada hizi, Baba Mtakatifu Francisko amethibitisha juu ya uzinduzi wa sanamu mara tu amalizapo tukio hili kwamba ni kielekeza cha mada kutoka katika kifungu cha Barua ya Waebrania kisemacho: msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua (Eb 14,2). Sanamu hii kubwa na udongo wa mfinyanzi inawakilisha kikundi cha wahamiaji wa tamaduni tofauti na nyakati tofauti za kihistoria. Aidha Baba Mtakatifu amefafanua sababu ya kupenda kazi hiyo ya kisanaa na kuiweka katika uwanja wa Mtakatifu Petro kwamba, ili kuwakumbusha watu wote juu ya changamoto ya kiinjili inayohusu suala la ukarimu.
Wito wa kusali kwa ajili ya nchi ya Camerun ili waweze kuwa na suluhisho la kudumu
Hali kadhalika Mara baada ya sala ya Malaika wa Bwana, Baba Mtakatifu Francisko amekumbusha kwamba tarehe 30 Septemba 2019 nchini Camerun utafunguliwa Mkutano wa majadiliano ya kitaifa kwa ajili ya kutafuta muafaka wa kipeo kigumu ambacho kwa miaka ya hivi sasa kinasumbua nchi hiyo. Kwa kuhisi ukaribu wa mateso na matumaini ya watu wapendwa wa Kameruni Baba Mtakatifu Francisko amewaalika watu wote wa Mungu kusali ili majadiliano hayoyaweze kuzaa matunda na kupata suluhisho la amani ya kweli na ya kuduma kwa ajili ya faida ya wote. Mama Maria Malkia wa Amani atuombee.