Baba Mtakatifu Francisko amesema kuwa mchezo ni mkondo maalum kwa ajili ya kuhamasisha amani na umoja Baba Mtakatifu Francisko amesema kuwa mchezo ni mkondo maalum kwa ajili ya kuhamasisha amani na umoja  

Papa Francisko:mchezo ni mkondo maalum kwa umasishaji wa amani!

Katika mkutano karibu wajumbe 176 wa Shirikisho la Kimataifa la Hockey kwenye barafu,Baba Mtakatifu Francisko tarehe 27 Septemba amekumbusha juu ya Kanisa kupongeza michezo kwa ajili ya kuhamasisha ujasiri,uvumilivu na kwamba sheria zinaepusha kuangukia katika machafuko.

Na Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Tarehe 27 Septemba 2019 katika salam za Baba Mtakatifu Francisko alipokutana mjini Vatican  na Shirikisho la Kimataifa la mchezo wa Hockey kwenye barafu  amebainisha juu ya Kanisa kupongeza  mchezo kama uwanja ambao unaweza kuhamasisha fadhila ya busara, unyenyekevu, ujasiri, uvumilivu na ushuhuda wa kukutana na hali halisi nzuri na ya furaha. Katika mkutano karibu na wajumbe 176 wa Shirikisho la Kimataifa la mchezo wa Hockey, Baba Mtakatifu amethibitisha kwamba Mchezo ni mkondo kwa dhati  maalum wa kuhamasisha amani na umoja.

Na wakati huo huo anamekumbusha umuhimu wa kisheria na kuheshimu washindani.Tabia za  kisasa wakati mwingine zinapelekea shughuli za michezo kwenye njia mbaya, japokuwa inabidi kuzingatia kwamba sheria zipo kwa ajili ya kuhudumia ili kufikia lengo lake kwa kuepuka kudumbukia katika machafuko. Wanariadha huheshimu mchezo mzuri sio tu wanapofuata sheria, lakini pia wanapofuata haki na heshima kwa wapinzani wao ili washindani wote waweze kushiriki kwa amani kwenye mchezo huo. 

Baba Mtakatifu akikumbuka ugeni uliomtembelea mwezi Mei mwaka huu wa shirikisho wakati wa kutolewa idhini ya kanuni zilizosasishwa, anathibitisha furaha yake ya kwamba kamati mpya ya maadili iliingizwa. Kama mchezo wa timu, Hockey ni mfano mzuri pia mchezo ambao unaweza kujifafanua kwa maana ya kukaa pamoja hata katika fursa ya furaha ya kukutana kati ya watu wa Nchi Tofauti kwa mfano kukutana na mashindano ya michezo duniani. Kwa njia hiyo mchezo ni nafasi ya kukua na katika maendeleo fungamani. Kwa upande mwingine, mchezo kwa kawaida unasaidia watu kuwa bora zaidi ndani mwao na kukuza uhusiano wa kirafiki.

Ki ukweli kufanya mazoezi ya hockey kwenye barafu inahitaji nguvu na ustadi, usawa, kwa kufuata maelekezo, kuanguka na kuamka tena  baada ya  kuteleza na  kuanguka. Baba Mtakatifu kwa maana hiyo amewatia moyo ili lengo la viongozi wa mchezo wa  Hockey kwenye barafu usiwe tu ni kudhibiti sheria, lakini ni kuifanya ujumuishe na kuonekana ulimwenguni kote. Na ndiyo hiyo njia ambayo wote wanaalikwa kuifuata,amehitimisha.

27 September 2019, 13:30