Papa anakazia kuhamasisha udugu wa kweli duniani!
Baba Mtakatifu Francisko tarehe 6 Juni ametuma ujumbe kwa askofu Jean-Claude Boulanger wa Bayeux-Lisieux,Ufaransa kufuatia na maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 75 tangu majeshi ya Marekani walipofika Normandy tarehe 6 Juni 1944 ili kuwakomboa dhidi ya utawala wa Kinazi.Papa anakazia kuhamasisha udugu wa kweli duniani unaojikita juu ya utamaduni wa makutano na majadiliano.
07 June 2019, 09:31