Papa amemkubuka Mwenyeheri Maria Guadalupe Ortiz de Landàzuri
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya sala ya Malkia wa mbingu,amekumbusha waamini na mahujaji wote waliokusanyika katika uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican tarehe 19 Mei 2019 ya kwamba Jumamosi huko Madri ametangazwa Maria Guadalupe Ortiz de Landázuri, kuwa mwenyeheri ambaye alikuwa ni mlei mwaminifu wa Shirika la Opus Dei. Aliweza kutoa huduma kwa furaha kwa ndugu huku akiunganisha na mafundisho na kutangaza Injili. Ushuhuda wake ni mfano kwa wanawake wakristo wanaojikita katika jamii na katika utafiti wa kisayansi. Baba Mtakatifu amewaomba watu wote wampigie makofi mwenyeheri mpya Guadalupe!
Mwenyeheri Maria Guadalupe Ortiz de Landàzuri alikuwa ni maarufu katika tafiti za sayansi ya kemia na ambaye aliweza kuunganisha taaluma yake na Neno la Mungu katika shughuli yake ya kisayansi. Na zaidi aliweza kujenga upendo kwa Mungu na jirani!
Salam kwa mahujaji wote
Baba Mtakatifu mara baada ya kumkumbuka mwenyeheri mpya pia ametoa salam mbalimbali kwa mahujaji kutoka duniani akianza na Italia, Mexico, California, Haiti; waamini kutoka Cordoba,Hispania, waamini wa Viseu Ureno na wanafunzi kutoka Pamplona na Lisbona. Aidha amewakumbuka washiriki wa kozi ya wahusika wa jumuiya ya Mtakatifu Egidio kutoka pande zote za dunia na wengine wengi na kwa wote wametakia matashi mema na baraka ya Jumapili. Wasisahau kusali kwa ajili yake!