Mara baada ya sala ya Malaika wa Bwana tarehe 7 Aprili 2019,Papa anawataka waamini wawe wajasiti katika ushuhuda wa Yesu na Injili yake Mara baada ya sala ya Malaika wa Bwana tarehe 7 Aprili 2019,Papa anawataka waamini wawe wajasiti katika ushuhuda wa Yesu na Injili yake 

Salam za Papa baada ya sala ya Malaika wa Bwana

Papa Francisko,mara baada ya tafakari na sala ya Malaika wa Bwana amewasalimia waamini na mahujaji wote na ameawataka wote wawe wajasiri katika ushuhuda wa Yesu na Injili.

Baba Mtakatifu Francisko anathibitisha kwamba kwa kujipatanisha kwa mara nyingine tena, msamaha unatupatia amani na kutufanya tuanze historia iliyo pyaishwa. Kila uongofu wa kweli ni matazamio ya wakati mpya wa maisha mapya, maisha mazuri na maisha yaliyo huru dhidi ya dhambi na kuwa na  maisha ya ukarimu. Hatuna hofu ya kuomba msamaha kwa Yesu, kwa sababu yeye anatufungulia mlango wa maisha mapya. Bikira Maria atusaidie kushuhudia wote upendo wa uhuruma ya Mungu ambaye ni katika Kristo anaye tusamehe na kufanya maisha yetu yawe mapya, akitoa fursa na  uwezekano mpya wa kujipyaisha daima!

Ujasiri katika ushuhuda wa Yesu na Injili yake

Mara baada ya sala ya Malaika wa Bwana tarehe 7 Aprili 2019 Baba Mtakatifu Francisko amewasalimia waamini na wote mahujaji kutoka pande zote za dunia, zaidi kama vile wanafunzi kutoka nchi ya Austria na Ufaransa. Aidha wanafunzi kutoka Bologna Genova, hata  Torino na Vercelli. Wazo limewaendea vijana wa kipaimara kutoka Settignano, Scandicci, na wengine kutoka jimbo la Saluzzo,Italia waliosindikizwa na Askofu  wao  Cristiano Bodo. Anawataka wote wawe wajasiri katika ushuhuda wa Yesu na Injili. Kwa kupokea  kipaimara wanapaswa wakue daima kwa ujasiri na wawe wajasiri. Amewakumbuka vijana wengine wadogo wenye umri wa miaka 14 kutoka Milano, waamini kutoka Pescara, Napoli na Terni. Kwa wote amewatakia Dominika njema na zaidi wasisahau kusali kwa ajili yake.

08 April 2019, 10:10