Papa:Pasaka inakaribia na tukiishi kipindi hiki kwa ukamilifu!
Baba Mtakatifu mara baada ya tafakari ya katekesi yake kwa waamini na wahujaji waliofika katika uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican kuungana naye tarehe 10 Aprili 2019 amewasalimia. Hata hivyo katika tafakari imekuwa ni mwendelezo wa sala ya Baba yetu, baada ya sehemu ya kuomba Mungu Mkate wa kila siku, na kujikita leo hii na sala ya maombi kwa Bwana kuhusu msamaha wa dhambi kama alivyo fundisha Yesu: “utusamehe makosa yetu kama tunavyo wasahamehe waliotukosea” (Mt 6,12).
Salam kwa mahujaji na waamini, vijana, wagonjwa na wanandoa wapya
Ametoa salam kwa mahujaji wote kutoka pande zote za dunia. Bila kuwasahau vijana, wazee,wagonjwa na wanandoa wapya. Kadhalika amewasalimia watawa wanao udhuria Kozi ya Umoja Wamama wakuu wamashirikia ya kitawa nchini Italia na Kitivo cha Kipapa cha elimu ya sayansi. Aidha na kuwakumbusha kuwa,“tunakaribia kuhitimisha safari ya Kwaresima. Mwanga na faraja za Pasaka ya Bwana zinakaribia! Tuombe, ili kuwa na hisia za Kristo na kuishi kwa ukamilifu katika siku za mateso na utukufu wake”.