Papa Francisko atabaruku Altare ya Parokia ya Mtakatifu Giulio,Roma!
Na Sr. Angela Rwezaula- Vatican
Baada ya mikutano na makundi mbalimbali ya Parokia ya Mtakatifu Gulio na kuungamisha baadhi ya watu, Baba Mtakatifu Francisko Jumapili, tarehe 7 Aprili 2019, ameongoza liturujia ya kutabaruku Altare ya Kanisa hili pamoja na kuadhimisha mafumbo ya Kanisa. Ni maadhimisho yenye utajiri mkubwa wa liturujia lakini hakufanya mahubiri. “Piteni katika Malango ya Bwana kwa utenzi wa neema na nyimbo za shukrani, ndiyo maneno aliyotamka Baba Mtatifu Francisko wakati wa kufungua Mlango wa kuingia katika Kanisa la Mtakatifu Giulio, huko Monteverde, ikiwa ni parokia ya 19 alizotembelea tangu kuanza huduma yake ya kichungaji kama khaarifa wa mtume Patro. Hili ni Kanisa lililokarabatiwa na kufunguliwa mara baada ya miaka 3. Baba Mtakatifu kabla ya kuanza misa takatifu, kama kawaida yake amweza kuwaungamisha vijana watatu na mama mmoja.
Papa hakutoa mahubiri
Katika liturujia ya kutabaruku Altare,wamenyunyizia maji na baadaye ya kusomwa Injili, na Baba Mtakatfu Francisko hakutoa mahubiri, badala yake amebaki kwa kimya cha sala akiwa ameinamisha kichwa chake. Baada ya sala ya Nasadiki ambayo ni imani ya kikristo na kusoma litania ya watakatifu, wameweka chini ya altare Masalia ya watakatifu ya Mtakatifu Yohane Bosco, Margherita Maria Alacoque pamoja na Mtakatifu Maria Goretti. Hii yote imewezekana kutokana na wanaparokia kushirikiano kwa pamoja kwa mika mitatu ili kukamilisha ukarabati wa Kanisa hili kwani paa liliporomoka na kuharibi Altare hiyo.
Maji, mafuta na mwanga
Mafuta ya krisma yaliyo barikiwa yametumika kupataka altare nzima ya Kanisa la Mtakatifu Giulio. Mikono yake imegusa jiwe kubwa na ambalo ni msingi hakika, unaokumbatia meza ambayo inatoa sadaka ya Ekaristi. Vile vile amefukizia ubani, na arufu ikajaza Kanisa, kama harufu ya Kristo ambayo Kanisa linaitwa kueneza ulimwenguni kote. Altare hiyo aidha imefunikwa na kitambaa cheupe lakini kikiwa juu na mwanga wa mishumaa, ambayo inataka kutafakari mwanga wa dunia ambao Yesu, anaungaza kwa watu wote. Baadaye vimeletwa vipaji, kwa Baba Mtakatifu ambavyo ni maji na divai, mkate na kuongeza kikapu cha matunda. Mwisho wa maadhimisho hayo, Paroko wa Parokia ya Mtakatifi Giulio, padre Dario Frattini mwanashrika wa Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili ameelezea furaha yao kwa niaba ya jumuiya nzima kutembelewa na Baba Mtakatifu Francisko. Amemwahidi kumsindikiza Baba Mtakatifu kwa sala za kila siku.
Paroko ametoa shukrani kwa Papa kuitembelea parokia
Anamshukuru kwa zawadi ya kufika na zaidi ya kutabaruku Kanisa na Altare. Kabla ya ziara hiyo, amethitisha kwamba wamejandaa kwa sala na kwa maana wao ni watu wa Mungu ambao wako katika mchakato wa safari kuelekea kwa Bwana. Zawadi ya Parokia kwa Baba Mtakatifu ni mchango mdogo ulio kusanywa kwa wiki nne za Kwaresima kwa ajili ya Caritas . Huu ni mpango wao kwa ajili ya watu wasio kuwa na makazi.