Papa anawashukuru sana kwa kile wanachofanya!
Na Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, kabla ya kuondoka, aliwasalimia watu wote wanaojikita katika hali halisi ya mapokezi ya wahamiaji ambao wameunganika katika Jumuiya ya Domus huko Sacrofano Roma, akiwatia moyo wa kuendelea mbele na kuwakumbusha kuwa ni hatua ndogo inayofanya safari kubwa ya historia. Maneno yake: kabla ya kuondoka ninapenda kumshukuru kila mmoja wenu kwa kile mfanyacho: hatua ndogo… ni hatua ndogo lakini ambayo inafanya safari kubwa ya historia. Njoo mbele! Msiogope, jipeni moyo! Na Bwana awabariki. Asante. Na pia kuhusiana na mahubiri yake Baba Mtakatifu Francisko, Rais wa Chama cha Migrantes,Monsinyo Guerino Di Tora, amefafanua kuwa ni ishara ya ukaribu na umoja, sababu ya kupyaisha matumaini na ushauri.
Wahudumu wamemshukuru Papa
Kadhalika katika furaha hiyokubwa na utambuzi wa kutembelewa na Baba Mtakatifu katika mkutano huo, imeonesha kwa shauku kubwa na wahudumu wote walei na watawa wanaojikita katika vituo mbalimbali vya hali halisi ya kukaribisha, walio kuwapo katika maadhimisho ya Ekaristi Takatifu, wakati wa ufunguzi wa Mkutano unaongozwa na mada: Huru dhidi ya hofu. Ni mkutano ulioandaliwa na Chama cha Migrantes, Caritas ya Italia na Kituo cha Astalli katika Mkutano wa siku mbili kuanzia tarehe 15 -17 Februari 2019. Ziara hii ilikuwa na tabia ya kifaragha kwa washiriki hao tu.