Papa:Jikabidhi kwa Mama Maria na Mtakatifu Yosefu
Sr. Angela Rwezaula -Vatican
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya katekesi yake, amewasalimia mahujaji wote kutoka sehemu mbalimbali za dunia, wakiwemo makundi mbalimbali ya maparokia, vijana na chama cha Kitaifa cha waathirika wa vita vya kiraia.
Vile vile mawazo yamemwendea kwa vijana, wazee, wagonjwa na wanandoa wapya. Baba Mtakatifu Francisko anasema: Katika sikukuu ya Kuzaliwa kwa Bwana iliyo karibu, hata kwa mwaka huu, usiku huo uweze kuamsha nyoyo zetu wote upendo wa Mungu kwa binadamu, kwa maana Yesu hakujibakiza, na akaweza kukomboa maisha ya asili ya binadamu katika ujio wake. Baba Mtakatifu anaombea wote na ili kujikabidhi kwa Mama Maria na Mtakatifu Yosefu, ili waweze kutufundisha kwa namna ya kukaribisha zawadi kubwa ya namna hii, yaani Emanuel Mungu pamoja nasi.