Tafuta

Mara baada ya salam kutoka kwa Kardinali Bechara Boutros Rai, patriaki wa Antiokia ya Kimaronite,Baba Mtakatifu Francisko amezungumza na walei zaidi ya 50 wa Chama cha Wamaronite Mara baada ya salam kutoka kwa Kardinali Bechara Boutros Rai, patriaki wa Antiokia ya Kimaronite,Baba Mtakatifu Francisko amezungumza na walei zaidi ya 50 wa Chama cha Wamaronite 

Papa anashukuru nchi ya Lebanon kwa makaribisho ya wakimbizi!

Tarehe 20 Novemba 2018, Baba Mtakatifu Francisko amekutana na wajumbe wa Chama cha Wamaronite, mara baada ya kuwapokea na kuzungumza na maaskofu wa Lebanon na diaspora ya Maronite katika fursa za hija ya kitume. Amewahimiza waendelee na msimamo wao katika ubunifu kama ndugu kati ya wakristo na waislam, washiite na Sunni

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Jumanne tarehe 20 Novemba 2018, Baba Mtakatifu Francisko, amekutana mjini Vatican na wajumbe wa Chama cha Wamaronite kutoka nchini Lebanon ambapo amewashukuru sana Jumuiya ya Walebanon kwa sababu ya kuwa na uwezo wa kuwatunza na kuwa na msimamo kati ya wakristo na waislam na kwa ajili ya ukarimu wa kuwapokea zaidi ya milioni moja ya wakimbizi kutoka pande zote za nchi za Mashariki ambazo ziko katika moto wa vita.

Ametamka hayo katika hotuba yake bila maandishi, ambapo amezungumza na wajumbe hao katika ukumbi wa Clementina wakiwa ni Wanachama wa Wamaronite  na viongozi wa nchi ya Lebanon,mara baada ya kuzungumza na na maaskofu 35 ambao ni  wa Kanisa la Upatriaki wa Antiokia ya Wamaronite, wanaojikita  katika utoaji wa huduma ya kichungaji katika  Jumuiya ya Lebanon, lakini hata wakihudumia waamini wengine wengi kutoka diaspora mbalimbali.

Waamini na maskofu na ndiyo wanatoa utambuzi bora wa jumuiya

Mara baada ya salam kutoka kwa Kardinali Bechara Boutros Rai, patriaki wa Antiokia ya Kimaronite, Baba Mtakatifu Francisko amewalekea  zaidi ya walei 50 wa Chama  hicho kwa kusisitizia kwamba ni wazo zuri la kusindikizwa na maaskofu, kwa maana hiyo inawezekana kujua kwa undani zaidi jumuiy hiyo. Hata hivyo kama kawaida yake ya vichekesho hakukosa kwatania akiongeza kusema:“na hivi waamini wanaweza kuchambua maaskofu!” Baba Mtakatifu ameongeza kusema: “Nimeambiwa kwamba nitakutana na watu karibia arobaini kuwasalimia, lakini sasa nimeona ongezeko zaidi la watu kutoka  Lebanon!”  “Asante kwa ujio wenu na kwa wingi wenu!”

Asante kwa sababu ya msiamamo kati ya wakristo na waislam

Akiendelea na shukrani, amewashukuru jumuiya ya Walebanon kwa ajili ya kile wanachofanya nchini humo. “Kwa ajili ya kutunza na kuwa na  msimamo, na kwamba  msimamo huo wa kiubunifu ni wa nguvu kama mpanzi, kati ya Wakristo na Waislam na Wasuuni na Washiite; ni msimamo ambao ni wa kizalendo na kindugu” amesisitiza. Aidha “kwa ajili ya ukarimu na moyo wa mapokezi ya wakimbizi ambapo amethibithisha kuwa ni zaidi ya milioni moja. Asante sana!”. Na mwisho Baba Mtakatifu Francisko  anamwomba Bwana ili awabariki wote, faimilia zao nchi zao , watoto wao na wakimbizi wao.

20 November 2018, 16:49