Papa Francisko awasalimia watu wote nchini Brazil
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Katika Sinodi inayoendelea mjini vatican , kuhusu vijana, imani na mang’amuzi ya miito, tarehe 11 Oktoba 2018, Askofu Vilsom Basso, wa Jimbo la Imperatriz (Brasil) alitengeneza video ya Papa akiwa na kijana msikilizaji kutoka nchini Brazil katika fursa ya Sikukuu ya Maria wa Aparecida ambaye ni Msimamizi wa nchi ya Brazil, siku ambayo inaadhimishwa kila tarehe 12 Oktoba ya kila mwaka.
Papa akiwa na sanamu ndogo mkononi ya Maria wa Aparecida
Papa akiwa na sanamu ndogo mkononi ya Maria wa Aparecida amezungumza kwa lugha ya kispanyola kwamba: “ Kwa watu wa Brazil, salam zangu za pendo ziwafikie ninyi nyote katika Sikukuu ya Mama Yetu wa Aparecida. Kila mmoja wenu anawaweza kukutana naye katika moyo, kama vile wavuvi, walivyokutana naye kwenye mto. Tafuteni maji ndani ya mioyo yenu na mtapata, kwa sababu yeye ni Mama. Na yeye anaweza kutusindikiza". "Mnikumbuke katika sala zenu".