Papa anasema watoto na wazee ni waathirika wa kubaguliwa Papa anasema watoto na wazee ni waathirika wa kubaguliwa 

Siku ya Viziwi Duniani:Papa anasema ushirikishwaji uwe mtindo!

Ikiwa umefikia mwaka wa 60 wa Siku ya Viziwi duniani, Papa Francisko katika ujumbe wake anasema,“ tunaalikwa pamoja kwenda kunyume na maono ya sasa, hasa kupambania hawali yote katika kutetea haki ya kila mwanamme na mwanamke ili apate hadhi. Na katika kesi hiyo familia ndiyo iwe mstari wa mbele kupyaishao hisia ya mawazo na maisha

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Ujumbe wa kuelezea ukaribu wakati anasubiri Mkutano wao, ndiyo sababu ambayo Papa Francisko ameandika ujumbe wake  kwa Chama cha Kitaifa cha Viziwi (E.N.S) ambacho kimejikita katika kupambana na ubaguzi na kuhamasisha thamani ya maisha wakati wa kuadhimisha mwaka 60 wa Kimataifa Duniani kwa viziwi. Chama hicho kinajikita kwa kuanzisha mambo mengi yanayohusu mshikamano.

Jitihada, sadaka , mapambano ya kila siku

Katika Ujumbe wa Chama cha Kitaifa cha Viziwi (E.N.S) Papa Francisko anaandika: “ni historia iliyoundwa na watu ambao wameamini katika umoja, katika mshikamano  na katika ushikirishano wa pamoja, kwa nguvu ya kuwa jumuiya ndani ya safari ya muda mrefu na nyenye maendeleo, ambayo haikosi sadaka na mapambano ya kila siku. Ni historia ya yule ambaye hakukata tamaa na kuendelea kuamini katika  kujitegemea kwa  watu viziwi. Hii ni matokeo mazuri, Baba Mtakatifu, akiwa anafikiria  watu wengi viziwi na familia zao ambao, wanakabiliwa na changamoto ya ulemavu, na kwamba hawahisi tena kuwa peke yao”.

Watoto na wazee ni waathirika wa kubaguliwa

Hata hivyo katika ujumbe wa Papa Francisko anatazama pia maendeleo makubwa yaliyofikia kwa mantiki nyingi, lakini wakati huo huo, hata  kuenea kwa  “utamaduni wa hatari na usiyokubalika, kwa sababu ya mgogoro wa kupungua maadili ya kibinadamu ambayo kwa sasa haifai tena kwa maana ya kwamba haiweki mtu kuwa kitovu , bali inatafuta maslahi ya kiuchumi, madaraka  na matumizi hovyo (taz Esort. ap. Evangelii gaudium, 52-53)."

Watu wenye udhaifu  ni miongoni mwa “waathirika wa utamaduni huu”, anasisitiza Papa, hasa “watoto “ambao wana shida ya kuweza kushiriki katika maisha ya shule” na “wazee” ambao hupata upweke na kuachwa, “vijan” ambao hupoteza maana yao ya  maisha na wanajiona kuibiwa wakati wao endelevu na  ndoto zao bora”.Ameandika Baba Mtakatifu.

Thamani ya kutengeneza chama

Papa Francisko amesisitizia pia juu ya thamani ya kutengeneza na kuwa mwanachama. “Ninyi si jumla ya watu, lakini mmejiunga ili kuishi na kuonesha mapenzi ya kuwasindikiza na kuwasaidia wale, ambao, kama ninyi  wako katika shida lakini  hawali ya yote ni wabebaji wa mali isiyo na kifani na thamani ya kibinadamu. Leo hii kuna haja kubwa ya kuishi na furaha na kujitolea katika mshikamano: kuwa na umoja wa kukutana, uzoefu wa kubadilishana, mafanikio na kushindwa, kuunganisha rasilimali, yote haya huchangia kuongezeka urithi wa mwanadamu, kijamii na utamaduni wa watu”.

Hebu twende kinyume cha mawazo ya sasa

Baba Mtakatifu amewaomba kwa hakika waende kinyume na mawazo ya sasa, na ili kupambania hadhi ya mwanaume na mwanamke, kupokea na kujiwezesha mwenyewe. Changamoto ni ile ya kujumuishwa na  kuwapokea ambayo ndiyo iwe  hisia na utamaduni  katika sheria na serikali zisikose  kuwa sababu ya sasa ya dhati katika kutoa msaada. Kuna haki za kuhakikishia pamoja na vizuizi vya dhati vinavyopaswa kushinda: “Ni lazima tujitoe nafsi zetu”, anaandika Papa, “kuvunja vikwazo vyote vinavyozuia uwezekano wa uhusiano na mkusanyiko wa uhuru na kufikia utamaduni na utendaji halisi wa kushirikishwa na  hii inatumika katika jumuiya za kiraia na jumuia ya Kanisa.

Umuhimu wa maono ya Kanisa

Papa ametoa hata mafanikio yaliyopatikana katika ngazi ya  kijamii na kitaaluma kwa wanachama wengi wa E.N.S. ambao pia wanashiriki katika muktadha wa Kanisa, Papa anasema: “ jinsi gani nilivyo na furaha sana wakati ninapoona kuwa ninyi , pamoja na watu wengine wenye ulemavu, kwa nguvu ya  ubatizo wenu mnafikia  malengo hayo hata ndani ya Kanisa, hasa katika uwanja wa uinjilishaji! Mfano huo unageuka kuwa  kichocheo kwa jumuiya za Kikristo katika maisha yao ya kila siku”.

Hitimisho la ujumbe wake ni ushirikiano katika kila jimbo  kati ya  watu viziwi na wahudumu wa wakichungaji walioandaliwa kwa ushirikiano kamili na hisia kamili. “Kwa sababu hiyo  anaandika, huduma ya kiuchungaji inayojumuisha, inahitajika katika parokia, vyama vya kitume  na mashuleni”. Kazi nyingi zimefanyika na mengi bado yanatakiwa kufanywa, anasisitiza Papa, “kwa kukuza watu viziwi ili  kushinda kutengwa kwa familia nyingi na kuwakomboa wale ambao bado wanahusika na ubaguzi usiokubaliwa”.

28 September 2018, 14:58