Rambirambi kutoka kwa Papa kufuatia kifo cha Rais wa Vietnam
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Kufuatia kifo cha Rais wa Vitnam Tran Dai Quang, Papa Francisko ametuma salam za rambirambi. Anaonesha masikitiko yake na kuwahakikishia maombi yake kwa rais wa Vietnam, Tran Dai Quang, aliyekufa akiwa na umri wa miaka 61. Rais Tran Dai Quang alichaguliwa kunako tarehe 2 Aprili 2016.
Ziara yake
Tarehe 23 Novemba 2016 alipata fursa ya kukutana na Papa Francisko. Katika maongezi yao, yaliyokuwa yametolewa na vyombo vya habari Vatican yanaonesha mahusiano mema yaliyopo baina ya Vatican na nchi ya Vietnam, kwa kuongozwa na roho ya umoja katika mazungumzo na msimamo wa pamoja, na katika kutafuta zana muhimu ili waweze kuendelea zaidi katika ulewanao na walionesha pia ushirikiano kati ya Kanisa na serikali kwa mantiki nyingi za kijamii mahalia.