Papa: Wekezeni katika elimu kwa ajili ya vijana waafrika!
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Afrika ni tajiri na utajiri mkubwa wenye thamani zaidi ni vijana. Ni katika ujumbe wake kwa njia ya video ambao imeandaliwa na Mtandao wa Dunia kwa ajili ya sala ya Papa ambayo ni maombi kwa mwezi wa Septemba 2018.
Kusali kwa ajili ya elimu na kazi kwa ajili ya vijana waafrika
Baba Mtakatifu akiendelea na ujumbe wake kwa njia ya video anakumbuka kuwa, vijana wanayo haki ya kupata elimu, “ wanapaswa waweze kuchagua, hasa kwa kuacha kushindwa na matatizo au kubadili matatizo yakawa fursa”. Baba Mtakatifu anakumbusha kuwa, ni lazima kuwekeza kwa ajili ya elimu yao ili kuhakikisha kwamba wanapata wakati endelevu wa Afrika na kuunda uwezekano wa nafasi za ajira kwa vijana katika nchi zao asilia.
Ukosefu wa ajira na utoro shuleni ni dharura ya kweli
Kwa mujibu wa takwimu ya Shirika la Kazi Ulimwenguni (ILO), linathibitisha kuwa mwaka 2017, nchi za Afrika chini ya Jangwa la Sahara, inaonesha ukosefu wa ajira kwa asilimia 12,9% ya vijana wa Afrika kati ya umri wa miaka 15 na 24. Wakati huohuo Unesco inakadiria kwamba, mwaka jana pia karibia asilimia 60% ya vijana wa Afrika, kati ya umri wa miaka 15 na 17 hawakwenda shuleni!