Papa Francisko kijikabidhi kwa Mama Maria Mkuu Afya ya Waroma kabla ya Ziara yake ya kitume nchi za Kibaltiki Papa Francisko kijikabidhi kwa Mama Maria Mkuu Afya ya Waroma kabla ya Ziara yake ya kitume nchi za Kibaltiki 

Papa:Sala ya Papa katika Kanisa la Mtakatifu Maria Mkuu

Siku mbili kabla ya kuanza ziara ya kitume, Papa Francisko alikwenda kama kawaida yake katika Kanisa Kuu la Mama Maria Mkuu ili kusali katika picha ya Mama Maria Afya ya Waroma, kama inavyothibitishwa na Msemaji Mkuu wa Habari Vatican Bwana Greg Burke

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Kama kawaida yake ya Papa Francisko kabla ya kuanza ziara yake ya kitume, hata mchana wa tahe 20 Septemba 2018, alikwenda katika Kanisa kuu la Mtakatifu Maria Mkuu na kupiga magoti kusali mbele ya Picha ya Mama Maria Afya ya waroma. Amefanya hivyo ikiwa ni katika kuanza ziara yake ya 25 ya kitume katika nchi za kibaltiki ambazo ni Lithuania, Latvia na Estonia, kuanzia tarehe 22- 25 Septemba 2018.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

21 September 2018, 12:53