Tafuta

Papa ameitisha Mkutano wa Marais wa Mabaraza ya Maaskofu duniani kote mwezi Februari 2019 Papa ameitisha Mkutano wa Marais wa Mabaraza ya Maaskofu duniani kote mwezi Februari 2019 

Papa atakutana na marais wa mabaraza ya Maaskofu duniani kote!

Mshikamano wa dhati umepyaishwa asubuhi ya tarehe 12 Septemba 2018 kwa Papa kutoka kwa Baraza la Makardinali 9 washauri kwa kile ambacho kimetokea katika wiki hizi za mwisho. Habari zilizotolewa na Vatican wakati wa kufunga Baraza hilo umetangazwa Mkutano na Papa na Marais wa Mabaraza ya Maaskofu duniani mjini Vaticvan mwezi Februari 2019

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Baba Mtakatifu Francisko, atakutana mjini Vatican na Marais wa Mabaraza ya Maaskofu Katoliki duniani kote kuanzia tarehe 21-24 Februari 2019, ili kuongea juu ya namna ya  kuzuia manyanyanyaso ya kingono dhidi ya watoto na watu wazima waathirika. Hayo yameleezwa na Kaimu Msemaji mkuu wa vyombo vya habari Vatican, Paloma Garcia Ovejero, wakati wa kikao kidogo, mara baada ya Mkutano wa Baraza la Makardinali washauri wa Papa (C9) ambapo hata Papa Francisko alikuwapo katika shughuli hiyo ya mkutano. Pamoja na hayo, Papa pia amempongeza Kardinali Sean Patrick O’ Malley, mara baada ya kukutana naye  na kusasishwa juu ya kazi inayoendelea ya Tume ya Kipapa kwa ajili ya ulinzi wa watoto.

Katika Mkutano huo  makardinali wote 9 wameonesha kupendezwa na mafanikio ya Mkutano wa IX wa Familia Duniani, uliofanyika hivi karibuni Mjini Dublin Ireland. Katika Kikao cha Baraza la Makardinali (C9) kwenye sehemu ya kwanza, liyofunguliwa  Jumatatu tarehe  10 Septemba,walianza na tafakari ya kina  kwa  mtazamo wa pamoja kuangalia  kazi ya muundo wenyewe wa Baraza hilo, kwa kuzingatia hata umri wa baadhi ya wajumbe katika Baraza. Pamoja na hayo hawakutoa habari zaidi, japokuwa wametoa taarifa juu ya mkutano wa (C9) ujao ambao utafanyika tarehe 10-12 Desemba 2018 ambayo walikuwa wameombwa na Papa Francisko

Ikumbukwe mkutano huo ulianza tarehe 10 Septemba mjini Vatican, wa Baraza la washauri wa Papa akiwemo hata Baba Mtakatifu Francisko. Huo ni mkutano wa XXVI wa Baraza la Ushauri la Makardinali. Baraza la Ushauri la Makardinali ambalo linaitwa C9 liliundwa kwa utashi wa Baba Mtakatifu Francisko ilikushirikiana katika majukumu ya huduma ya Kanisa na ushirikiano kwa ajili ya  mageuzi ya Vatican. Shughuli yao inaongozwa na Papa mwenyewe. Hiki ni  Kikao cha XXVI tangu kuanza kwake kunako tarehe 1-3 Oktoba 2013.

Kwa miaka hii mitano sehemu kubwa ya shughuli imejikita katika mtazamo wa Katiba mpya ya mageuzi ya Vatican yenye kauli mbiu ya muda  "Praedicate evangelium" yaani "Hubirini Injili".  Makardinali Washauri 9 wameweza kwa sasa kumkabidhi Papa rasimu ya muda , ili kuweza kutoa marekebisho ya muundo na kusomwa na wanasheria. Mkutano huo umeudhuriwa na makardinali sita, kwa maana ya kutoweza kufika Kardinali Francisco Javier Errázuriz Ossa, Askofu mkuu mstaafu wa Santiago ya Chile, Kardinali Laurent Monsengwo Pasinya,Askofu mkuu wa  Kinshasa na George Pell, Rais wa Sektreatarieti ya Uchumi Vatican

12 September 2018, 16:30