Mwenyeheri wa Romania aliyeuwawa mwaka 1958
Baba Mtakatifu amekumbuka kuwa tarehe 22 Septemba huko Neampţ nchini Romania atatangazwa Mwenye heri Veronica Antal, mwamini mlei msekulari wa Shirika la Mtakatifu Francisko aliyeuwawa kutokana na kukiri imani yake kunako mwaka 1958
Sr Angela Rwezaula - Vatican
Mara baada ya tafakari yake ya Siku, Baba Mtakatifu ametoa salam kwa waamini wote na mahujaji kutoka pande zote za dunia, waliofika katika viwanja vya Mtakatifu Petro mjini Vatican, tarehe 19 Septemba 2018.
Na katika salam hizo, Baba Mtakatifu amekumbuka kuwa tarehe 22 Septemba 2018 huko Neampţ nchini Romania atatangazwa Mwenye heri Veronica Antal, mwamini mlei msekulari wa Shirika la Mtakatifu Francisko aliyeuwawa kutokana na kukiri imani yake kunako mwaka 1958. Baba Mtakatifu amesema, tumshukuru Mungu kwa ajili ya mwanamke jasiri ambaye alitoa maisha yake akishuhudia upendo wa kweli kwa ajili ya Mungu na ndugu!
19 September 2018, 14:57