Papa katika Madhabahu, ameomba kujenga madaraja na siyo kuta!
Sr. Angela Rwezaula - Vatican
Madhabahu yenye jina la Mater Misercordiae, inawakilisha kile kinachobaki cha ukuta wa kisazamani ili kulinda mji wa Vilnius. MJi huo uliharibiwa kunako mwaka 1799 na kubaki limesimama Lango kuu mahali ambapo tangu wakati ule hadi sasa waliweka picha ya Bikira wa Huruma. Matembezo ya Kanisa la Mama Maria ilikuwa ndiyo hatua ya kwanza ya Papa Francisko kwa waamini wa Lithuania alasiri ya Ijumaa tarehe 22 Septemba 2018.
Picha ya Mama inajionesha kwa kila kwa kila mmoja Yesu
Picha ya Mama Maria wa Vilnius haina mtoto, bali imepambwa yote, ni mama wa wote, amesema Papa Francisko, wakati wa hotuba yake ya pili Katika Madhabahu ya mama Maria na kuongeza, yeye kwa kila mmoja anaonesha uso wa Mtoto wake Yesu. Iwapo picha ya Yesu inawekwa kama mhuri kwa kila moyo wa binadamu, kila mwanaume na kila mwanamke, ina uwezo wa kukufanya kukutana na Mungu”.
“Tunapojifungia sisi binafsi kwasababu ya kuogopa wengine, tunapojenga kuta na vizingiti, tunaishia kukosa bahati ya kupata Habari njema ya Yesu ambaye anapeleka historia na maisha ya wengine, anathibitisha Baba Mtakatifu. Kadhalika anasisitiza:”Tumejenga vizingiti vya nguvu nyingi kipindi kilichopita, lakini leo hii tunahisi mahitaji ya kutazamana uso kwa uso na kutambuana kama ndugu na kutembea pamoja tukigundua na kufanya uzoefu na furaha na amani ya tunu msingi wa kindugu.
Kuwa na msimamo dhatibiti wa makutano kati ya wote
Shukrani kwa uwezekano wa mawasiliano na mzunguko wa ulio huru, anaendela Papa , watu wengi wanatembelea kila siku Madhabahu hiyo , kutoka nchin Lithuania, wapoland, waurusi ya magharibi na mashariki, wakatoliki na waorthodox. Jinsi gani ilivyo nzuri kuona uwezekano huo wa kusafiri kutoka sehemu moja kufika sehemu nyingine, ungeweza hata kuwa ndiyo wa kuwekwa msimama thabiti wa makutano na mshikamano kati ya wote na kuweza kufanya izunguke zawadi nyingi zilizopokewa kutoka kwa Mungu bure, kuondokana na ubinafsi na kuweza kuwazawadia wengine, kwa kupokea mara nyingine tena uwepo na utofauti wa wengine kama zawadi na utajiri katika maisha yetu.
Mama anatamani kuunganisha familia ya kibinadamu
Hali halisi ya sasa, inampeleka Baba Mtakatifu kufikia kutaja masuala ya migogoro, mivutano, chuki na uadui. Na hivyo Baba Mtakatifu Francisko amesema kuwa, Mama wa Huruma anatamani kuunganisha familia ya binadamu na kwa kila mtu anamwamba “ Tafuta ndugu yako”. “Leo hii wanatusubiri watoto na familia wakiwa na majeraha yanayotoa damu; si madonda yale ya Lazaro, katika somo la Injili, yale ni madonda ya Yesu; ya kweli na dhati, pia ya uchungu wao na giza nene linalowasonga, wanaomboleza ili sisi tuwe mwanga wa kuponya kwa njia njia ya upendo”.
PapaFrancisko akiendalea tena na wazo lake kwa mama Maria ametoa ushauri wa “kuomba msaada kwa ajili ya kujenga jumuiya yenye uwezo wa kutangaza Yesu Kristo, kwa ajili ya nchi, yenye uwezo wa kwapokea wote, (…) Nchi ambayo inachagua kujenga madaraja na si kuta na inayopendelea huduma na si kuhukumu”.
Kusali pamoja fungu moja la Rosari
Mwisho wa hotuba yake, Papa Francisko amewaalika waamini kusali fungu moja ya Rosari, wakitafakari tendo la tatu la matendo ya furaha, yaani Yesu anazaliwawa Betlehemu. Ni watoto na familia ambao wamekuwa mstari wa mbele kuongoza Salam Maria katika lugha ya kilithuania….
Baadaye imefuata wimbo wa salam Malkia na sala katika lugha ya kilatini iliyosomwa na Papa Francisko, na baadaye Papa Francisko ametoa zawadi yake katika Altare ya Mama wa Huruma, ambayo ni rozari ya dhahabu. Na mwisho kuwabariki kama hitimisho la mkutano huo. Nje ya madhabua alikuwa akisubiriwa watu wengi wakimsalimia wakati anaondoka kwenda kukutana na vijana waliokuwa wanamsubiri karibu na uwanja wa Kanisa Kuu Katoliki la Vilnius.