Ajali ya maporomoko huko Raganello  Calabria - Italia Ajali ya maporomoko huko Raganello Calabria - Italia 

Papa: Maombi na ukaribu kwa waathirika wa Raganello Calabria

Mwisho wa katekesi yake Baba Mtakatifu wazo lake limetazama janga jingine la siku hizi huko Raganello Carabria, Italia kutokana na mapomoko ambapo watu 10 wamepoteza maisha. Amekumbusha pia siku ya tarehe 22 Agosti kuwa ni siku ya kumbukumbu ya Bikira Maria Regina na kuomba kusindikizwa kwa sala katika Ziara yake ijayo tarehe 25-26 Agosti

Sr. Angela Rwezaula - Vatican

Katika salam zake nyingi alizotoa Baba Mtakatifu kwa kwa lugha mbalimbali mwishoni mwa katekesi yake Baba Mtakatifu wazo lake limetazama janga jingine lilitokea siku za hivi karibuni huko Raganello Carabria nchini Italia. Janga hili hili limewapoteza watu 10 katika moja ya maporomoko ya maji, wakiwa katika mzunguko wa kutembelea maporomoko hayo kama sehemu ya mchezo wakati wa kiangazi na kusababisha majeruhi akiwemo hata mtoto. Hawa ni wanawake 6 na wanaume 4.

Ni janga ambalo lingekuwa pia hatari zaidi na kwa maana yalikuwa ni makundi mawili jumla yao wakiwa 36, ambao walikuwa wameganyika wakitembelea eneo hilo bila kuwa na habari ya hatari ambayo wangekutana nayo! Hadi sasa watu 23 wameokolewa ambapo kati yao kuna mtoto msichana mwenye umri wa miaka 8 ambaye hali yake ni mbaya kulingana na taarifa za vyombo vya habari.

Kutokana na hayo, watu wanaoteseka na msiba huo, Baba Mtakatifu Francisko anawaonesha ukaribu wake wa maombi kwa  familia zao , majeruhi  na kuwakabidhi watu waliopoteza maisha katika huruma ya Mungu .

Papa kuomba sala kwa ajili ya ziara yake ya kitume nchini Ireland

Kadhalika ametoa salam zake kwa vijana, wazee, wagonjwa na wanandoa wapya.  Baba Mtakatifu pia anasema kuwa katika Liturujia ya leo hii ni Sikukuu ya Bikira Maria Rejina. Kwa maana hiyo Mama wa Mungu awe kimbilio katika kipindi kigumu na kuwafundisha kupenda mwanaye kwa upendo wake wa dhati kama alivyompenda. Baba Mtakatifu amewaomba pia ala kwa ajili ya ziara yake ya kitume  ijayo tarehe  25-26 Agosti  na kwamba, katika fursa ya Mkutano wa Familia duniani, uweze kuwa  kipindi cha neema na kusikiliza sauti ya wanafamilia wakristo duniani. Bwana awabariki nyote.

22 August 2018, 17:13