Daraja limeanguka huko Genova Italia, tarehe 14 Agosti 2018 na kusababisha vifo na majeruhi wengi.  Daraja limeanguka huko Genova Italia, tarehe 14 Agosti 2018 na kusababisha vifo na majeruhi wengi.  

Papa amesali kwa ajili ya waathirika wa daraja la Genova

Papa Francisko mara baada ya sala ya Malaika wa Bwana amesali kwa ajili ya majanga na mateso duniani, kwa namna ya pekee, kuanguka kwa daraja la Genova nchini Italia, ambalo limesababisha vifo na majeruhi wengi. Amemkabidhi uchungu na maombolezo ya watu kwa Mama Bikira Maria Mpalizwa Mbinguni

Sr. Angela Rwezaula – Vatican

Ndugu wapendwa Kaka na dada, kwake  Mama yetu mfariji wa wenye uchungu, ambaye tunamtafakari katika utukufu wa mbingu, ninataka kumkabidhi uchungu na maombolezo wote  ambao katika sehemu mbalimbali za dunia wanateseka kimwili na kiroho. Mama yetu wa mbinguni aweze kuwafariji na kuwapa nguvu, ujasiri na utulivu!

Ni mwanzo wa maombi ya Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya takafakari ya Malaika wa Bwana  kwa waamini na mahujaji waliofika katika viwaja vya Mtakatifu Petro mjini Vatican, wakati Kanisa katoliki linaadhimisha Sikukuu ya Kupalizwa kwake Mbinguni Mama Maria ifanyikayo kila ifikapo tarehe 15 Agosti ya kila mwaka.

Kuanguka kwa daraja huko Genova, Italia.

Akiendelea na maelezo anakumbuka kwa namna ya pekee waliojaribiwa na janga la kuanguka kwa daraja  tarehe 14 Agosti huko Genova Italia na kusambabisha waathirika wengi na wasiwasi mkubwa wa watu. Kwa maana hiyo anawakabidhi wote katika huruma ya Mungu watu wote  waliopoteza maisha  na kuonesha  ukaribu wa kiroho na maombi kwa ajili ya familia zao, majeruhi na watu wengi ambao kwa sasa wamerundikana pamoja kutokana na kuharibiwa nyumba , aidha hata wengine walioguswa na wanateseka kutokana na tukio hilo. Anawaalika wote kuungana naye katika sala na kuomba kwa  ajili ya waathirika na kwa ajili ya wapendwa wao kwa  sala ya Salam Maria…

Na mwisho amesalimia watu wote Roma, mahujaji kutoka maeneo mbalimbali ya nchi dunani kote, na kuwashukuru uwepo kwa  kuwatakia sikukuu njema ya Bikira Maria Mpalizwa  lakini pia wasiwasahau kamwe kusali kwa ajili yake!

15 August 2018, 15:14